Nafasi Ya Matangazo

May 18, 2016



 Mkulima wa  Shahiri pamoja na maofisa kilimo wa TBL wakikagua mashamba




Wabunge wa Kamati ya BIashara na Kilimo walipotembelea mashamba ya wakulima wa zao la Shahiri hivi karibuni.

Mkulima wa Shahiri Peter Nade akiwa amesimama kwenye trekta lake ni mmoja wa wakulima waliofanikiwa chini ya mpango huu
 **************
UTEKELEZAJI wa mpango wa kufanya kazi kwa kushirikiana na wakulima wadogo wadogo ujulikanao kama Go Farming ambao umeanza kutekelezwa  na kampuni ya TBL Group kwa wakulima wa zao la Shahiri kanda ya Kaskazini mwa Tanzania umesaidia kuongeza ajira ikiwemo kuboresha maisha ya wakulima.

Afisa Mwandamizi wa TBL Group anayesimamia mpango huo Bw.Optat Morrice  amesema jana mjini Arusha kuwa mpango wa Go Farming  awamu ya kwanza unatekelezwa katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro mbali na wakulima unanufaisha watanzania zaidi ya 3,000 wanaojipatia ajira katika utekelezaji wake.

Aliyataja makundi ya wawaonufaika na mpango huu kuwa ni vibarua wanaofanya kazi mashambani kwa kupuliza dawa mashambani,madereva wa matrekta wanaolima mashamba na kuvuna,vibarua wa kupakia mazao na kuyashusha,wasafirishaji na watengenezaji na magunia ya kupakia mazao.

Alisema Mbali na wanaonufaika katika hatua  mbalimbali za utekelezaji wakulima wa zao la Shahiri katika mikoa ya Kaskazini ya Arusha na Kilimanjaro tayari  wameanza kuonja matunda ya ushirikiano huu kwa kuwa wanawezeshwa kuendesha kilimo cha kisasa,kupatiwa pembejeo,mbegu na wataalamu wa kutoa ushauri na wanakuwa na soko la uhakika kwa ajili ya kuuza mazao yao,hali ambayo imebadilisha hali zao za maisha kuwa bora.

Morrice alisema lengo kubwa la mpango huu ni kuinua maisha ya wakulima wadogowadogo,kuongeza kasi ya kukua uchumi na kujenga mfumo mzuri na endelevu wa  kupata malighafi kwa ajili ya viwanda kampuni mama ya TBL Group ya SABMiller vilivyopo kwenye nchi mbalimbali barani Afrika.

“Mpango wa Go Farming haulengi kunufaisha wakulima wa Shahiri pekee bali pia wa mazao mengine kama mtama na mihogo na katika siku za usoni wakulima wa zao la mahindi watawezeshwa pia na inategemewa hadi kufikia mwaka 2020 zaidi ya wakulima nusu milioni watakuwa wamewezeshwa sehemu mbalimbali duniani ambako kampuni imewekeza na mamilioni ya wananchi watajipatia riziki kutokana na kufanya kazi za utekelezaji wake”.Alisema Morrice.

Aliongeza kuwa matarajio ya mafanikio ya mpango huu katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020 yanaonyesha kukua kwa asilimia 44 katika nchi 10 ambako umeanza kutekelezwa na inakadiriwa kuwepo ongezeko la uzalishaji wa mazao kutoka tani 300,000 kufikia zaidi ya tani 600,000.

Mpango huu wa kampuni kutegemea kupata malighafi kutoka  hapa nchini umeungwa mkono na serikali za nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania kwa kuwa unalenga kuinua hali za maisha za wananchi hasa wakulima ambao wana hali duni,hali hii imepelekea baadhi ya nchi kuipunguzia kodi ya zuio kampuni inapofanya uzalishaji kwa malighafi zilizonunuliwa ndani ya nchi .

Hivi karibuni Kamati ya Bunge ya Viwanda,Biashara ya Mazingira ilipata fursa ya kutembelea wakulima wa zao la Shahiri wanaoshirkiana na TBL Group na baadhi ya wajumbe wa kamati hii walipongeza mpango huu wa kushirikiana na wakulima kuwa utaweza kuinua sekta ya kilimo nchini kwa haraka na kuboresha maisha ya wakulima.

Huu ni mfano wa uwekezaji wenye faida kwa watanzania kwa kuwa unaeleta mabadiliko kwenye jamii na kubadilisha maisha ya wananchi wengi kuwa bora.
Posted by MROKI On Wednesday, May 18, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo