Nafasi Ya Matangazo

September 01, 2015


 Meneja Mkuu wa Double Tree hotel Ndugu Ian Mclachlan Akimkabidhi  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Msaada wa Magoro 80 .Akipokea Msaada huo Mkuu wa Wilaya Mh Makonda ameushukuru Uongozi wa Msaada huo.Kutoka Hotel ya Double Tree ya Jijini Dar es salaam.Msaada huo umekabidhiwa na Mkuuwa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda.Kituo Hicho kinacholea Watoto na vijana wa Mitaani na wanaoishi katika Mazingira Magumu kina Jumla ya Watoto Pamoja na Vijana 120 Kilianzishwa Mnamo mwaka 1998  Kwa lengo la Kuwasaidia watoto waliokosa Malezi na Huduma Mbalimbali za Kijamii.Kituo Hicho kinapatikana Kimara Suka pamoja na Kijiji cha Mazizini msata wilayani Bagamaoyo kinakabiliwa na Changamoto Mbalimbali hivyo Uongozi wa Kituo Hicho kinawaomba Watu binafsi na Wafadhili Mbalimbali kujitokeza kuwasaidia

  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda akimkabidhi  Mkurugenzi wa Kituo cha Watoto wetu tanzania Ndugu Evans Tegete Msaada  uliotolewa na Uongozi wa Double Tree Hotel .
Kituo cha Watoto wetu Tanzania leo kimepokea Msaada wa Magodoro 80 .Mkuu wa Wilaya Mh Makonda ametaka Uongozi wa Kituo cha Watoto Wetu tanzania Msaada huo Kuwanufaisi watoto wa Kituo hicho na Kuutunzaili uweze kusaidia watu wengi zaidi.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Katika Picha na Meneja Mkuu wa Double Tree hotel Ndugu Ian Mclachlan  (kushoto) Pamoja na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Hotel ya Double tree Ndugu Florenso Kirambata

 Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Hotel ya Double tree Ndugu Florenso Kirambata Akieleza jambo wakati  Kukabidhi Msaada huo.Ikumbukwe Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Hotel ya Double Ndiye aliyefanikisha Kupatikana kwa Msaada huo Mara baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Alipotembelea Kituo cha Watoto wetu Tanzania na Kujionea Changamoto zilizokuwa zinawakabili watoto hao hao ndipo alipoamua Kumshirikisha Mkurugenzi huo ambaye Ameweza Kuushawishi uongozi wa Hoteli Hiyo kutoa Msaada huo ikiwa ni sehemu Msaada kwajili ya Jamii inayoizunguka Hotel hiyo.
Mkurugenzi wa Kituo cha Watoto wetu tanzania Ndugu Evans Tegete Akitoa Neno la shukrani mara baada ya Kupokea Msaada huo ambapo aliushukuru Uongozi wa Double tree hotel kwa Msaada huo Pamoja na Mkuu wa Wilaya aliyetembelea Kituo hicho na Kujionea Changamoto zinazowakabili.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda Katika Picha na Meneja Mkuu wa Double Tree hotel Ndugu Ian Mclachlan  (kushoto) Pamoja na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Hotel ya Double tree Ndugu Florenso Kirambata
Posted by MROKI On Tuesday, September 01, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo