Nafasi Ya Matangazo

May 01, 2015

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Dk Mustafa Ali Garu akitiliana saini ya makubaliano ya Mrai wa Uchimbaji wa Kisima katika maeneo ya Bamani na Mwenyekiti wa Tanzania Youth Icon, Ndg Abdullah Miraji Othman, mradi huo utaharimu shilingi za kitanzania milioni mia tatu, utilianaji wa saini hiyo umefanyika katika Ofisi za ZAWA Mabuluu
 WANANCHI wa Jimbo la Kikwajuni wakishuhudia utilianaji wa saini ya makubaliano ya Mradi wa Uchimbaji wa wa kisima cha Maji Safi na Salama kwa Wananchi wa jimbo hilo.
MKURUGENZI wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Dk Mustafa Ali Garu akibadilishani Mikatabani ya makubaliano ya Mradi wa Uchimbaji wa Kisima katika maeneo ya Bomanii Unguja Mradi huo utagharimu shilingi milioni Mia tatu, akibadilisha na Mwenyekiti wa Tanzania Youth Icon, Ndg Abdullah Miraji Othman, mradi huo utaharimu shilingi za kitanzania milioni mia tatu, utilianaji wa saini hiyo umefanyika katika Ofisi za ZAWA Mabuluu.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar Mhe. Eng.Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kutiliana saini ya Makubaliano ya Mradi wa Uchimbaji wa Kisima, mradi unaosimamiwa na Tanzania Youth Icon.
Waandishi wa habari wakiwa katika ukumbi wa Afisi za ZAWA Mabluu Unguja wakifuatilia makubaliano hayo.
Mheshimiwa Meya ya Mji wa Zanzibar Mhe Khatib Abdurahaman Khati na Diwanj wa Kikwajuni Mhe Mahboob wakishuhudia utilianaji wa saini hiyo ya makubaliano ya Mradi wa Maji Awamu ya Pili kwa Jimbo hilo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Dk Mustafa Ali Garu akizungumza wakati wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini ya Makubaliano ya pande hizo mbili yaliofanyika katika Afisi Kuu ya ZAWA  Mabluu Zanzibar.
Waheshimiwa wakifuatilia hafla hiyo ya utilianaji wa Saini ya Mradi wa Uchimbaji wa kisima cha Maji Safi na Salama kwa Wananchi wa Jimbo la Kikwajuni, mradi huo unaosimamiwa na Tanzania Yuoth Icon na Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA)
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe Eng. Hamad Yussuf Masauni, akimkabidhi mashine ya Pump ya Maji ya Mradi wa Kwanza wa Kisima cha Kaburi Kikombe, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar Dk Mustafa Ali Garu,  ambao uko katika hatua za mwisho ya ufungaji wa Pump hiyo na tayari kwa kutowa huduma ya maji kwa wananchi wa Jimbo lake.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe Eng. Hamad Yussuf Masauni, akimkabidhi  Pump ya kuvutia maji kwa ajili ya kisima kipya cha Kaburi Kikombe, Mkurugenzi  Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Dk. Mustafa Ali Garu.kwa ajili ya Mradi wa Kwanza wa Uchimbaji wa Kisima cha Kaburi Kikombe ambao uko katika hatua za mwisho ya ufungaji wa Pump hiyo na tayari kwa kutowa huduma ya maji kwa wananchi wa Jimbo lake.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Dk Mustafa Ali Garu, akitowa shukrani kwa Mlezi wa Jumuiya ya Tanzania Youth Icon (TAYI) kwa ushirikiano wa Taasisi hiyo na ZAWA, katika jitihada zake za kukamilisha Mradi Mkubwa wa Kisima huko Kaburi Kikobe na kutiliana saini ya makubaliano ya Mradi wa Pili wa Uchimbaji wa Kisima katika eneo la bomani Unguja ukiwa na thamani ya shilingi milioni mia tatu.
Posted by MROKI On Friday, May 01, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo