Nafasi Ya Matangazo

February 15, 2013



Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) anaeshughulikia masuala ya Siasa, Dk. Julius Rotich (wapili kushoto) akizungumza leo katika Mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Uteketezaji wa Silaha ndogo ndogo litakalo fanyika Ukonga chini ya usimamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania. Pamoja nae kutoka kushoto ni Mtaalam wa Masuala ya Amani wa EAC, Leonard Onyonyi, Mkuu wa Kitengo cha Silaha Ndogo ndogo wa Jeshi la Polisi Tanzania, SACP. Modest Mwauzi na Mtaalam wa Masuala ya Habari wa EAC, Sukhdev Chatbar.

Mbali na zoezi hilo la uteketezaji wa silaha pia kutakuwapo na Utilaji saini ya itifaki ya Ulinzi na Amani kwa nchi za Jumuia hiyo.Mgeni Rasmi anataraji kuwa Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal.

 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya ndani na nje ya Jumuia ya Afrika Mashariki wakifuatilia mkutano huo.
Mtaalam wa Masuala ya Amani wa EAC, Leonard Onyonyi, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusiana na zoezi hilo pamoja na kutiliana saini kwa Itifaki ya kufungwa kwa zoezi hilo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) anaeshughulikia masuala ya Siasa, Dk. Julius Rotich.

Mkuu wa Kitengo cha Silaha Ndogo ndogo wa Jeshi la Polisi Tanzania, SACP. Modest Mwauzi akitoa maelezo juu ya maandalizi ya zoezi hilo.

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) anaeshughulikia masuala ya Siasa, Dk. Julius Rotich (katikati) akizungumza leo katika Mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Uteketezaji wa Silaha ndogo ndogo litakalo fanyika Ukonga chini ya usimamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania. Pamoja nae kutoka kushoto ni Mtaalam wa Masuala ya Amani wa EAC, Leonard Onyonyi, na Mkuu wa Kitengo cha Silaha Ndogo ndogo wa Jeshi la Polisi Tanzania, SACP. Modest Mwauzi.
Posted by MROKI On Friday, February 15, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo