Nafasi Ya Matangazo

July 22, 2024

  
Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Majid Mwanga  (watatu kulia) akipokea sehemu ya msaada wa magodoro, viti na meza kutoka kwa Meneja wa Benki Uhusiano wa Benki ya CRDB Kanda ya Nyada za Juu Kusini, Pascalia Bura, (katikati) kwa ajili ya Shule ya Msingi ya Majimoto (Shule Maalum), katika hafla ya makabidhiano hayo, yaliyofanyika mwishoni mwa wiki Wilayani ya Mpimbwe, mkoani Katavi. Wapili kulia ni Mbunge wa Mbunge wa Jimbo la Kavuu, Geophrey Pinda, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mpimbwe, Shamimu Mwariko (watatu kushoto) pamoja na viongozi wengine mbalimbali.
 *****************

Benki ya CRDB kupitia sera yake ya kurudisha kwa jamii sehemu ya asilimia moja ya faida yake, imeweza kutoa msaada wa magodoro 68 pamoja na viti 24 na meza 2 kwa matumizi ya wanafunzi wenye changamoto za usikivu na madawati 25 kwa ajili ya wanafunzi wenye changamoto ya uoni hafifu na viungo katika Shule ya Msingi ya Majimoto (Shule Maalum) , iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, mkoani Katavi.

Akipokea msada huo, Mkuu wa Wilaya ya Mlele anayesimamia pia Wilaya ya Mpimbwe, Majid Mwanga ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuona umuhimu wa kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutatua changamoto mbalimbali za elimu hapa nchini. Ameishuru Benki ya CRDB kwa msaada huo wa magodoro, viti pamoja na meza.

Msaada huo ni muendelezo wa programu maalumu ya benki hiyo iitwayo 'Keti Jifunze' yenye lengo la kuwawezesha wanafunzi kujifunza wakiwa wameketi katika mazingira mazuri na salama. Shule Maalum ni zile zinazohudumia wanafunzi wenye changamoto mbalimbali kama vile uoni, usikivu na viungo.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Majid Mwanga  (watatu kushoto), Mbunge wa Jimbo la Kavuu, Geophrey Pinda (watatu kushoto), Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mpimbwe, Shamimu Mwariko (wapili kulia), Meneja wa Benki Uhusiano wa Benki ya CRDB Kanda ya Nyada za Juu Kusini, Pascalia Bura (wapili kushoto) pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB na Halmashari wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wanafunzi Shule ya Msingi ya Majimoto (Shule Maalum) iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, mkoani Katavi.
Meneja wa Benki Uhusiano wa Benki ya CRDB Kanda ya Nyada za Juu Kusini, Pascalia Bura (watatu kushoto) akizungumza jambo wakati wa hafla ya kukabidhi magodoro, viti na meza


Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Majid Mwanga akizungumza katika hafla hiyo.




Posted by MROKI On Monday, July 22, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo