Waziri wa Habari, Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye
akizungumza wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wataalam
wa Mikoa na Halmashauri wa Tanzania Bara na Zanzibar kuhusu mfumo wa anwani
za Makazi na Postikodi kwa njia ya mtandao, katika ukumbi wa mikutano wa
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) leo tarehe 17 Januari, 2022, jijini Dar
es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi akizungumza wakati wa
ufunguzi wa semina ya kuwajengea uwezo wataalam
wa Mikoa na Halmashauri wa Tanzania Bara na Zanzibar kuhusu mfumo wa anwani
za Makazi na Postikodi kwa njia ya mtandao, katika ukumbi wa mikutano wa Shirika
la Mawasiliano Tanzania (TTCL) leo tarehe 17 Januari, 2022, jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa
Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Clarence
Ichwekeleza akimuonesha Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Kinondoni Cde, Harold
Maruma namna ya kupata postikodi ya kata
mbalimbali nchini kwa kutumia simu ya mkononi wakati wa semina ya kuwajengea
uwezo wataalam wa Mkoa wa Dar es Salaam
kuhusu mfumo wa anwani za Makazi na Postikodi iliyofunguliwa na Waziri wa Wizara hiyo, Nape Nnauye, Jijini
Dar es Salaam.
Mhandisi Jampyion Mbugi wa
Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari akiwasilisha mada ya kuwajengea
uwezo wataalam wa Mkoa wa Dar es Salaam
kuhusu mfumo wa anwani za Makazi na Postikodi
uliofanywa na Waziri wa Wizara hiyo, Nape Nnauye, Jijini
Dar es Salaam.
Muonekano wa picha ya pamoja
ya viongozi wakifuatilia ufunguzi rasmi wa semina ya
kuwajengea uwezo wataalam wa Mkoa wa Dar es Salaam
kuhusu mfumo wa anwani za Makazi na Postikodi
uliofanywa na Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (wa pili kushoto meza kuu), Jijini
Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara
ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Clarence Ichwekeleza
akitoa utambulisho kabla ya ufunguzi rasmi wa semina ya kuwajengea uwezo
Wataalam wa Mikoa na Halmashauri wa Tanzania Bara na Zanzibar kuhusu mfumo wa
anwani za Makazi na Postikodi
uliofanywa na Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Nape Nnauye (hayupo pichani) kwa
njia ya mtandao, katika ukumbi wa mikutano wa Shirika la Mawasiliano Tanzania
(TTCL) leo tarehe 17 Januari, 2022, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla
akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa semina ya kuwajengea uwezo wataalam
wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu mfumo wa anwani
za Makazi na Postikodi uliofanywa na Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari
Mhe. Nape Nnauye (hayupo pichani), Jijini,
Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye
akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Jim
Yonazi
wakati wa ufunguzi wa semina ya kuwajengea uwezo wataalam
wa Mikoa na Halmashauri wa Tanzania Bara na Zanzibar kuhusu mfumo wa anwani
za Makazi na Postikodi kwa njia ya mtandao, katika ukumbi wa mikutano wa
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) leo tarehe 17 Januari, 2022, jijini Dar
es Salaam.
Mkutano ukiendelea kwa njia ya mtandao.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye (aliyeketi
katikati) akiwa katika
picha ya pamoja na Watendaji wa Wizara hiyo baada ya kufungua
semina ya kuwajengea uwezo Wataalam
wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu mfumo wa anwani za
Makazi na Postikodi uliofanyika Jijini
Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya
Habari Mhe. Nape Nnauye (aliyeketi katikati) akiwa
katika picha ya pamoja na Wakuu wa Wilaya za Dar es Salaam (waliosimama nyuma) baada
ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo Wataalam
wa Mkoa huo
kuhusu mfumo wa anwani za Makazi na
Postikodi iliyofanyika
Jijini
Dar es Salaam.
************
Prisca Ulomi
na Paschal Dotto, DSM
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye amewataka wakuu wa mikoa nchini kusimamia vyema zoezi la utekelezaji wa uwekaji wa anwani ya makazi ili liweze kukamilika katika muda uliopangwa.
Akizungumza
katika ufunguzi ma mafunzo ya utekelezaji wa mfumo huo ambao unatekelezwa na
Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano, mafunzo ambayo
yalifanyika kwa njia ya Mkutano Mtandao (Video conference) Jijini Dar es Salaam,
yakihusisha Halmashauri 163 za Tanzania Bara na Mikoa 12 ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo ushiriki wa Wakuu wa Mikoa hiyo nawataalam wao, Waziri
Nape amesema kuwa utekelezaji wa jambo hilo ni muhimu kwani Sekta ya Mawasiliano
ni wezeshi kwa sekta nyingine nchini.
“Mawasiliano
ni Sekta muhimu na mtambuka kwani sekta zote zinategemea mawasiliano ili ziweze
kufanya kazi kwa ufanisi, zoezi la utekelezaji wa anwani za makazi ni jambo
ambalo litawasaidia wananchi kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa katika kujiletea
maendeleo”, amesema Waziri Nape.
Waziri Nape
alisema kuwa utekelezaji ni jambo muhimu ambapo Tanzania inatekeleza mfumo huo
kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Posta ya Mwaka 2003, Ilani ya Chama cha
Mapinduzi ya 2020 – 2025, Ibara ya 61(m) pamoja na miongozo ya Umoja wa Posta
Afrika na Umoja wa Posta Duniani ambapo Tanzania ni nchi mwanachama.
Utekelezaji
wa mfumo huo ni moja kati ya mikakati ya kuiweka nchi katika mfumo wa kidijitali
ili kurahishisha upatikanani wa huduma kwa wananchi pamoja na kurahisisha biashara
ya mtandaoni ambapo Serikali ya Awamu ya sita imedhamiria kuacha alama.
“Mradi huu ni
moja ya miradi ambapo Rais wa Awamu ya Sita, Mhe. Samia Suluhu Hassan
amedhamiria kuacha alama na utekelezaji wake ulitakiwa ufanyike kwa miaka mitano
lakini kwa sababu ya umuhimu wake mpaka mwezi Mei mwaka huu zoezi hili litakuwa
limekamilika”, Alisema Waziri Nape.
Aidha, Waziri
Nape alisema kuwa utekelezaji wa Anwani za makazi itakuwa ni zoezi ambalo litarahisisha
zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ambayo itafanyika Agosti mwaka
huu na itakuwa rahisi kwa sababu ya upatikanaji wa anwani za makazi.
Katika hatua
nyingine mafunzo hayo yalifunguliwa kwa mkoa wa Dar es Salaam ambapo Waziri Nape
aliwataka viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwaelimisha wananchi kwani
ndiyo wanaviongozi wengi katika mitaa mbalimbali nchini.
Waziri Nape
alieleza jinsi mkoa wa Dar es Salaam unahitaji utekelezaji wa haraka wa
utambuzi na uwekaji wa anwani za mitaa pamoja na nyumba ambapo kata 46 kati ya 102
ndizo zoezi hilo limetekezwa lakini kwa ujumla majina 85,728 ya barabara
yanahitajika na vibao milioni moja vya nyumba vinahitajika ili kazi hiyo ikamilike.
Akizungumza, awali
katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano
na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi, amesema kuwa mfumo wa anwani ya makazi
ni muhimu sana kwa wananchi.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye amewataka wakuu wa mikoa nchini kusimamia vyema zoezi la utekelezaji wa uwekaji wa anwani ya makazi ili liweze kukamilika katika muda uliopangwa.
“Zoezi hili tumelianza na linaendelea vizuri, Wizara inashirikiana vizuri na Serikali za Wilaya kuhakikisha kuwa zoezi na utekelezaji wa mfumo huu unafanyika kwa ufanisi mkubwa ili kuwawezesha wananchi kufanya kazi na kujiletea maendeleo”, Alisema Amour.
0 comments:
Post a Comment