Nafasi Ya Matangazo

June 28, 2021

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa, Filemon Namwinga (kulia), akikabidhi Hatimiliki za Kimila kwa baadhi yawakulima wa zao la chai ambao mashamba yao yamerasimishwa na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) kwa ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya hiyo. Jumla ya mashamba 220 yamerasimishwa katika vijiji vitano vya Ilamba, Lusing'a, Magome, Kidabaga na Ng'ang'ange. Anayeshuhudia kulia kwake ni Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini wa MKURABITA, Anthony Temu.

Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni Makao Makuu ya Halmashauri hiyo, baada ya wanufaika hao kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kuzitumia hati hizo kuweka dhamana kukopa fedha benki na taasisi zingine za fedha za kusaidia kuboresha miradi yao.



Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini wa MKURABITA, Anthony Temu akielezea umuhimu wakurasimisha ardhi pamoja na faida ya kuwa na Hatimiliki za Kimila wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wakulima hao. ambapo walifundishwa  jinsi ya kutunza kumbukumbu za mahesabu ya miradi yao, kupanga mipango ya miradi, kanuni za kilimo bora cha zao la chai, kujiunga na benki ili kupata fursa za mikopo, kuthaminisha mali na ufugaji wa nyuki.
  
Mmoja wa wakulima akifurahia kupata hatimiliki za kimila.
Mmoja wa wakulima akitoa maelezo kuhusu maisha na mambo ya kiuchumi wakati wa kukusanya dodoso.
Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, Emmanuel Mwakilema akitoa mafunzo kuhusu kanuni bora za kilimo cha zao la chai.

Wakulima wakipatiwa hatimiliki zao.
Baadhi ya Wakulima kutoka vijiji vitano wilayani Kilolo wakisikiliza kwa makini wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo.

Posted by MROKI On Monday, June 28, 2021 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo