Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisisitiza uwajibikaji kwa watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (hawapo pichani) alipoitembelea idara hiyo kwa lengo la kufahamu majukumu ya idara na kuhimiza uwajibikaji.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora alipoitembelea idara hiyo kwa lengo la kufahamu majukumu ya idara na kuhimiza uwajibikaji.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Mathew Kirama (wa pili kutoka kulia) akifafanua majukumu ya Idara yake kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (kulia) alipoitembelea idara hiyo kwa lengo la kufahamu majukumu ya idara na kuhimiza uwajibikaji.Watumishi wa umma wametakiwa kuwa tayari kufanya kazi mahali popote na
katika mazingira yoyote nchini ili waweze kuwahudumia wananchi ambao ndio
walengwa wakuu wa huduma zinazotolewa na Taasisi za Umma.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) alipokutana na watumishi
wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora kwa lengo la kufahamu majukumu ya Idara hiyo na
kuhimiza uwajibikaji.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, kitendo cha watumishi wa umma kuwa tayari
kufanya kazi mahali popote na katika mazingira yoyote bila kujali maslahi
binafsi kinaashiria uzalendo kwa Taifa na kinatoa haki kwa wananchi katika
maeneo yote hususan ya pembezoni kupata huduma bora wanayostahili.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa ameitaka Idara
ya Utawala wa Utumishi wa Umma kutorubuniwa na baadhi ya watumishi na waajiri
wanaoomba vibali vya uhamisho kwa maslahi binafsi hivyo kuathiri utoaji huduma
kwa umma.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa ameongeza kuwa, Idara hiyo inatakiwa kujiridhisha na
hoja zinazowasilishwa kuombea vibali vya uhamisho kama hoja hizo zina tija na
manufaa katika maendeleo ya Taifa.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesisitiza kuwa, watanzania wote wana haki sawa ya
kupata huduma bora bila kujali mazingira waliyopo hivyo, ni wajibu wa Idara
hiyo kuhakikisha kuwa uhamisho wa watumishi hauathiri mahitaji ya huduma kwa wananchi.
Awali,
akielezea majukumu ya idara yake, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa
Umma, Bw. Mathew Kirama amesema, Idara hiyo ina Sehemu ya Utawala wa Utumishi
wa Umma, Sehemu ya Watumishi Waandamizi na Sehemu ya Huduma na Ushauri wa Kisheria
ambazo kwa pamoja zinalenga kufanikisha uendeshaji wa utumishi wa umma kwa
kuwezesha Taasisi za Serikali kupata watumishi wenye sifa na weledi
unaohitajika kulingana na malengo yanayotekelezwa na Taasisi hizo.
Bw.
Kirama amefafanua kuwa, idara hiyo ina
jukumu la kutoa ushauri wa kitaalamu kwa waajiri na watumishi kuhusu sera, sheria,
kanuni na nyaraka mbalimbali za masuala ya ajira katika Utumishi wa Umma, kutoa
ushauri wa kitaalamu kuhusu masuala ya sheria ikiwa ni pamoja na kusimamia
taratibu mbalimbali zinazotawala utumishi wa umma.
Akizungumzia
suala la uhamisho, Bw. Kirama amesema, katika kuleta tija na ufanisi kwenye
utumishi wa umma, watumishi wa umma wanaruhusiwa kuhama ikiwa wamezingatia
sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo likiwemo sharti la kukaa kwenye
kituo kimoja cha kazi si chini ya miaka mitatu na uwepo wa nafasi iliyotengewa
fedha kwenye kituo husika. Aidha alieza kuwa, Serikali inaweza kumhamisha
mtumishi kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma katika
maeneo yenye upungufu wa watumishi.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) ameitembelea Idara ya Utawala wa
Utumishi wa Umma ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake katika Idara na Vitengo vya
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kuhimiza uwajibikaji.
0 comments:
Post a Comment