Nafasi Ya Matangazo

August 23, 2017

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia amewateua Makamu wa Rais wa zamani wa TFF, Athuman Nyamlani na Ahmed Mgoyi kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF.



Rais Karia ameteua kwa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo katika Katiba ya TFF ikiwa ni wiki moja baada ya kupatikana kwa viongozi wa shirikisho katika uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 12, mwaka huu.



Rais Karia aliwatambulisha viongozi hao kwenye Kikao cha Kamati ya Utendaji iliyofanyika Jumanne Agosti 22, mwaka huu jijini Dar es Salaam.



Katika kikao hicho pia Rais Karia alitumia fursa hiyo kutangaza viongozi wa kamati mbalimbali za TFF zikiwamo za kinidhamu na kisheria. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

Kamati ya Nidhamu: Mwenyekiti Tarimba Abbas, Makamu Mwenyekiti, Peter Hella wakati wajumbe ni Boniface Lyamwike, Dk. Bill Haonga na Kassim Dau.



Kamati ya Rufani za Nidhamu: Mwenyekiti ni Wakili Rahim Zuber Shaban; Makamu Mwenyekiti, Stella Mwakingwe wakati Wajumbe ni Abbas Mtemvu, Amani Mulika na Siza Chenja.



Kamati ya Maadili: Mwenyekiti ni Wakili Hamidu Mbwezeleni, Makamu Mwenyekiti ni Wakili Steven Zangira wakati Wajumbe ni Glorious Luoga, Walter Lungu na Amin Bakhressa.



Kamati ya Rufaa ya Maadili: Mwenyekiti ni Wakili Ebenezer Mshana; Makamu Mwenyekiti ni DCP. Mohammed Mpinga na wajumbe  ni Wakili Benjamin Karume, George Mayawa na ASP. Benedict Nyagabona.



Kamati ya Uchaguzi: Mwenyekiti ni Revocatus Kuuli; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Mohammed Mchengerwa; Wakili Edwin Mgendera; Wakili Kiomoni Kibamba na Wakili Thadeus Karua.



Kamati ya Rufani ya Uchaguzi: Mwenyekiti ni Kenneth Mwenda; Makamu Mwenyekiti ni Jabir Shekimweri na Wajumbe ni Wakili Rashid Sadalla, Irene Kadushi na Mohammed Gombati.



Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji: Mwenyekiti ni Elias Mwanjala; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Malangwe Mchungahela wakati Wajumbe ni Zakaria Hanspope, Robert Selasela, Goodluck Moshi, Mhandisi Issa Batenga na Hamis Semka.



Kamati ya Fedha na Mipango: Mwenyekiti ni Michael Wambura; Makamu Mwenyekiti ni Francis Ndulane na Wajumbe ni Almas Kasongo, Pascal Kihanga, Maximillian Tabonwa, Paul Bilabaye na Farid Abeid.



Kamati ya Mashindano: Mwenyekiti ni Ahmed Mgoyi; Makamu Mwenyekiti ni James Mhagama wakati Wajumbe ni Kenneth Pesambili, Shafii Dauda, Fortunatus Kalewa na Mhandisi Andrew Makota.



Kamati ya Ufundi: Mwenyekiti ni Vedastus Lufano; Makamu Mwenyekiti ni Issa Bukuku na wajumbe ni Sarah Chao, Ally Mayay, Michael Bundala, Omar Abdulkadir na Israel Mujuni.



Kamati ya Soka la Vijana: Mwenyekiti ni Khalid Abdallah; Makamu Mwenyekiti ni Lameck Nyambaya na Wajumbe ni Mohammed Aden, Ramadhani Nassib, Salim Kibwana na Vicent Majili.
Kamati ya Mpira wa Wanawake: Mwenyekiti ni Amina Karuma; Makamu Mwenyekiti ni Rose Kissiwa na Katibu wa Kamati hiyo ni Somoe Ng’itu wakati Wajumbe ni Zena Chande, Beatrice Mgaya, Sofia Tigalyoma, Zuhura Kapama na Nia Mjengwa.



Kamati ya Waamuzi: Mwenyekiti ni Saloum Chama; Makamu Mwenyekiti Joseph Mapunda wakati Wajumbe ni Nassib Mabrouk, Leslie Liunda na Soud Abdi.
Kamati ya Habari na Masoko: Mwenyekiti ni Dunstan Mkundi; Makamu Mwenyekiti ni Mbasha Matutu wakati Wajumbe ni Imani Kajura, Mgaya Kingoba, Godfrey Dilunga na Samson Mbamba.



Kamati ya Ukaguzi wa Fedha: Mwenyekiti ni Yahya Hamad; Makamu Mwenyekiti ni Athuman Nyamlani na Wajumbe ni Khalifa Mgonja, Japhary Kachenje, Jackson Songoro na Benesta Rugora.



Kamati ya Tiba: Mwenyekiti ni Dkt. Paulo Marealle; Makamu Mwenyekiti ni Dkt. Fred Limbanga Wakati wajumbe ni Dkt. Norman Sabun, Dkt. Lisobina Kisongo, Dkt. Eliezer Ndalama, Dkt. Elson Maeja na Violet Lupondo.



Kamati ya Futsal na Beach Soccer: Mwenyekiti ni Ahmed Mgoyi; Makamu Mwenyekiti ni Hussein Mwamba na Wajumbe ni Blassy Kiondo, Isaac Munisi, Didas Zimbihile na Aaron Nyanda.



Kamati ya Ajira: Mwenyekiti ni Issa Bukuku; Makamu Mwenyekiti ni Saloum Chama wakati Wajumbe ni Athuman Kihamia, Mtemi Ramadhani, Noel Kazimoto na Hawa Mniga.



Kamati ya Leseni za Klabu: Mwenyekiti ni Wakili Lloyd Nchunga; Makamu Mwenyekiti Wakili Emmanuel Matondo wakati Wajumbe ni Profesa Mshindo Msolla, Hamisi Kissiwa na David Kivembele.



Kamati ya Rufaa za Leseni: Mwenyekiti Wakili Dk. Damas Ndumbaro; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Alex Mngongolwa Wajumbe ni Meneja wa zamani wa Uwanja wa Taifa, Charles Matoke, Tumainiel Mlango na Ahmed Menye.
Posted by MROKI On Wednesday, August 23, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo