Nafasi Ya Matangazo

January 04, 2017




Katibu Mkuu wa wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Mbogo Futakamba (Katikati kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Menejimenti ya DAWASCO, baada yakumaliza kikao cha kumuaga katibu mkuu huyo (katikati kulia ) ni Afisa mtendaji mkuu wa Dawasco.


*******************
Katibu Mkuu wa wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Mbogo Futakamba amewataka wafanyakazi wa Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es salaam (Dawasco) kufanya kazi kwa ushirikiano, nidhamu pamoja na kuwa wabunifu katika kazi, ili kufanikisha utoaji wa huduma bora ya Majisafi na Majitaka katika jiji la Dar es salaam pamoja na Miji ya Kibaha na Bagamoyo mkoani Pwani.


Hayo yalizungumzwa katika kikao cha pamoja kilichoandaliwa na menejimenti ya Dawasco cha kumuaga Katibu Mkuu huyo ambaye anamaliza muda wake wa utumishi katika umma kisheria, kikao ambacho  kilichofanyika makao makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam.

Nawashukuru sana kwa ushirikiano wenu mzuri ambao umenipa heshima na kuniondolea aibu katika suala zima la Maji, ninawasihi muendelee kuwa na nidhamu pamoja na ubunifu katika kazi kwani mimi mwenyewe nilikuwa mbunifu”.

Aidha, ameipongeza Dawasco kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakifanya ikiwemo ya kudhibiti upotevu wa Maji kwa kiwango kikubwa kwa kuzuia mivujo kwa wakati na wizi wa maji katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam na Pwani.

Naye, Afisa Mtendaji mkuu wa Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es salaam (Dawasco), Mhandisi Cyprian Luhemeja amempongeza katibu mkuu huyo kwa ushirikiano na uaminifu mkubwa alionyesha kipindi chote cha utumishi wake, amemtakia heri na mafanikio katika maisha yake mapya anayokwenda kuyaanza.

Kwa niaba ya wafanyakazi wote, tunakushukuru sana mzee wetu kwa mchango wako mkubwa katika shirika kipindi chote cha utumishi wako, tumejifunza mengi kutoka kwako, sisi wafanyakazi wa Dawasco tunakuombea Baraka na mafanikio makubwa katika maisha yako mapya ya ustaafu”.

Posted by MROKI On Wednesday, January 04, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo