Nafasi Ya Matangazo

May 04, 2016

Konstebo Said Sengendu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kituo cha Ilala akitoa maelezo ya utumiaji wa vifaa mbalimbali vilivyopo katika magari ya kuzima moto na maokozi kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo,  Thobias Andengenye . (Picha na FC Godfrey Peter)
***********
Katika ziara hiyo Kamishna Jenerali alipata fursa ya kukagua mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula liliopo mkoa wa kinondoni kwa ajili ya kurahisisha upatikani wa huduma kwa askari.

Pia amesisitiza kufufua visima vya maji ya kuzima moto (fire hydrant) kwa kushirikiana na ofisi ya idara ya maji  ili kurahisisha kupatikana kwa maji yanapohitajika na jeshi la zimamoto na uokoaji.

Amesema kuwa kwa kushirikiana nao itasaidia kufufua visima vilivyokufa au kuingiliwa na makazi ya wananchi na kufanya zoezi la upatikanaji wa  maji ya  kuzima moto kuwa karibu na  wazimamoto watapata maji na kurudi kwenye tukio kwa haraka zaidi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (wa kwanza kushoto) akiongozwa na Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Kinondoni, Mrakibu Msaidi Peter Mabusi wakikagua mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula lililopo katika kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Lugalo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (aliyeketi kulia) akipokea taarifa ya utendaji kazi kutoka kwa Kamanda Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Kamishna Msaidi, Jesuald Ikonko alipotembelea kituoni hapa leo hii mapema asubuhi katika ziara ya kutembelea vituo vya zimamoto nchini.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye akipokea maelezo kutoka chumba cha mawasiliano namna ya upokeaji taarifa ya miito ya dharura . 
Posted by MROKI On Wednesday, May 04, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo