Nafasi Ya Matangazo

March 21, 2016

SHIRIKA la Majisafi na Majitaka jijini Dar es Salaam (DAWASCO) limewapiga faini ya shilingi milioni 17 raia wa China wanaofanya kazi kwenye wizara ya afya (Chinese medical team) baada yakubaini wizi mkubwa wa maji kwenye nyumba wanayoishi iliyopo mtaa wa Mtwara Oysterbay Jijini Dar es salaam.

Akizungumza kwenye eneo la tukio Meneja wa Dawasco Kinondoni, Judith Singinika alisema waliwabaini wizi huo baada ya kufanya operesheni maalum kwenye mtaa huo ya kubaini wizi wa maji ndipo walipofanikiwa kunasa nyumba hiyo ikiwa imeunganishiwa maji pasipo mita na kukuta imefungwa pampu kubwa ya kuvuta maji kutoka kwenye laini ya bomba kubwa.

“Dawasco tumewapiga faini raia wa China kiasi cha shilingi milioni 17 baada yakuwanasa wamejiunganishia huduma ya maji kinyume na utaratibu na laini inayopeleka maji ndani haina mita na imefungwa pampu kubwa yakuvuta maji wakati sio utaratibu hivyo tumeng’oa pampu na nakuwapiga faini,”alisema Singinika.

Singinika alisema raia hao wa china watalazimika kulipa fedha hizo ndani ya miezi 24 ambapo kila mwezi watalipa sh laki saba kwa dawasco.

Meneja huyo wa Dawasco amesisitiza kuwa operesheni hiyo yakukamata wezi wa maji kwenye maeneo tofauti ya ijini Dar es Salaam niendelevu na inatokana na agizo la Waziri wa maji na umwagiliaji, Gerson Lwenge ambapo alilitaka shirika hilo kukagua majengo yote makubwa pamoja na viwanda nakujiridhisha matumizi yake ya maji.


Dawasco inaendelea kuwasihi watu wote waliojiunganishia huduma ya Maji kiholela kinyume cha utaratibu kwenye nyumba za makazi, majengo makubwa pamoja na viwanda kujisalimisha nakutambuliwa kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa endapo wakibainika kwani ndio wanaolikosesha Shirika mapato.
Posted by MROKI On Monday, March 21, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo