Nafasi Ya Matangazo

June 16, 2015

  Sheikh Shaban Issa Bin Simba (78)  
(Picha hii ilipigwa 28/7/2014 Wakati wa Swala ya Eid El Fitir, viwanja vya Mnazi Mmoja). 

MWILI wa Mufti na Sheikhe Mkuu wa Tanzania, Sheikh Shaban Issa Bin Simba unatarajiwa kusafirishwa kesho mkoani Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Alhad Mussa Salum amesema swala ya marehemu itafanyika katika Msikiti wa Al Farouq Kinondoni jijiji Dar es Salaam asubuhi  na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na serikali.

Aidha taarifa kutoka kwa Mtoto wa marehemu Suleiman Issa Simba inasema kuwa Mwili wa marehemu utasafirishwa leo na kuzikwa leo hii  16/6/2015 Majengo mkoani Shinyanga majina ya saa 10:00 jioni. 
Awali palikuwa na mvutano baina ya familia na BAKWATA juu ya siku ya mazishi lakini familia imesisitiza wosia wa marehemu kuwa asicheleweshwe kuzikwa pindi mauti yakimfika.
Amesema marehem alikuwa akisumbuliwa na sukari,Shinikizo la Damu (BP)  pamoja na Figo.
Hata hivyo amesema kuwa jana (Jumapili) Mufti alifanyiwa oparesheni ya figo katika Hospitali ya TM Jijini Dar es Salaam na Mauti ya Mufti yamekuta majira ya saa3:45 leo asubuhi. 

SALAM ZA RAMBI RAMBI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Waislamu wote nchini na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania  (BAKWATA)) kufuatia kifo cha Sheikh Mkuu wa Tanzania  Mufti Sheikh  Issa Bin Shaaban Simba.
Marehemu Mufti amefariki  leo 15/6/2015 asubuhi katika hospitali ya TMJ – DSM alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa sukari na shinikizo la damu (pressure).
"Kifo kinaleta huzuni, hata hivyo Kifo hakizuiliki, hatuna budi kukikubali na ni wajibu wetu kumuombea Sheikh Mkuu kwa Mola wetu ampe mapumziko ya milele". Rais Kikwete ametuma salamu hizo za rambirambi kupitia kwa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salum.
"Nawaombea subra wana familia, ndugu, jamaa, waislamu wote na wana jamii kwani Mufti alikua kiongozi katika Jamii yetu'Rais amesema na kueleza kuwa "Kamwe mchango wake hautasahaulika katika jamii yote kwa Ujumla na hakika sote tutamkumbuka" ameongeza.
Marehemu alijiunga na BAKWATA mwaka 1968 na amekuwa mwalimu wa chuo katika mikoa mbalimbali ya Mwanza, Bukoba na Mwaka 1970 alikuwa Shekhe wa Mkoa wa Shinyanga.
Rais amemuelezea Marehemu Mufti kama mwalimu katika jamii ambaye alikua na uzoefu wa hali ya juu na mwenye kupenda dini yake na kuitumia kwa manufaa ya jamii iliyomzunguka
"Amekua mwalimu imara na mtu wa kutumainiwa na kutegemewa katika uislamu na jamii kwa ujumla, hakika tutamkumbuka siku zote' Rais Kikwete ameongeza.
Shekhe Issa Bin Shaaban Simba alikuwa na uzoefu  mkubwa ndani ya BAKWATA na  aliwahi kukaimu nafasi ya mufti kwa siku 90, baada ya kifo cha Mufti Hemed mwaka 2002.
Baada ya hapo akasimamia mchakato wa uchaguzi wa Mufti Mkuu na baadaye 2003 akachaguliwa kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania.
Mwenyezi Mungu ailaze roho yake pahali pema Peponi, Amina.
Posted by MROKI On Tuesday, June 16, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo