Nafasi Ya Matangazo

May 16, 2015

Hii ni sehemu ya barabara ya Tabata Kimanga ambayo imeharibiwa vibaya katika eneo la Tabata Chama jirani na Shule ya Msingi Darajani. Endapo mamlaka husika hazitafanya ukarabati wa haraka wa eneo hilo basi mawasiliano ya barabara kwenda au kutoka Tabata Kimanga yapo hatarini kukatika na watu kushindwa kwenda mjini au kurejea katika makazi yao. 

Eneo hilo liliwahi kuharibika na kujazwa kifusi katika mvua za msimu uliopita lakini ukarabati huo ulipaswa uende sambamba na uwekaji wa mawe na hata zege katika eneo hilo.
Posted by MROKI On Saturday, May 16, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo