Nafasi Ya Matangazo

December 22, 2014


Akiwa ana nyimbo za “Mwana” na “Kimasomaso” zikiongoza  katika vituo mbali mbali Africa, Alikiba aachia video ya “Mwana” iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu jana ,Ijumaa tarehe 19 Decemba 2014 kwa mamilioni ya mashabiki Africa na duniani. “Mwana” ni nyimbo ya kwanza  baada ya kufunga mkataba wake na kampuni ya Rockstar4000 Management na Rockstar Publishing.

Rekodi ya “Mwana” ni nyimbo ya kwanza kutoka kwenye albamu ya tatu ya Alikiba baada ya kutokuwa katika muziki kwa muda wa miaka mitatu. Alikiba alifafanua kwa kusema “ Hii ni album itayoonyesha kukua kwangu kimuziki na kuonyesha utofauti mbali mbali katika kipaji changu nilichojaliwa.”  

Alikiba alitoa kibali ili video ya “Mwana” iruke hewani jana “exclusively” kwa masaa 24 kwenye vituo vya televisheni vitano Africa katika vipindi maarufu kwenye vituo hivyo na kuwafikia mashabiki zaidi ya milioni 500 kwa pamoja.

 Vituo vya televisheni hivyo ni Clouds TV kuonyesha exclusive Tanzania, Nation TV kuonyesha exclusive Uganda, One Music Networks kuonyesha exclusive Cameroon, Angola, Ethiopia, USA na UK, Sound City kuonyesha exclusive Nigeria na Ghana na Citizen TV exclusive kwa upande wa Kenya, DRC Congo na Rwanda
Posted by MROKI On Monday, December 22, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo