Nafasi Ya Matangazo

September 23, 2014



Na Fadher Kidevu Blog
KIUNGO mshambuliaji  wa Simba Raphael Kiongera,huenda akalikosa pambano la watani wa jadi Simba na Yanga kutokana na maumivu makali ya goti.

Kiongera  alipata maumivu hayo Jumapili iliyopita wakati timu yake ikicheza na Coastal Union katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara uwanja wa taifa.

Daktari wa Simba Yassin Gembe,amesema vipimo alivyofanyiwa mchezaji huyo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili vimeonyesha tatizo hilo ni lamuda mrefu na litachukua wiki sita hadi miezi miwili ili liweze kupona na mchezaji huyo kurudi uwanjani.

Kamati ya usajili ya Simba imekuwa na sinto fahamu baada ya majibu ya vipimo hivyo kwa sababu mchezaji huyo hakufanyiwa vipimo wakati akisajiliwa kutoka KCB inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya.

Kiongera aliingia uwanjani dakika ya 66,kuchukua nafasi ya Mrundi Amisi Tambwe,lakini alilazimika kutolewa kwa machela dakika za nyongeza baada ya kugongana na kipa wa Coastal Union Shabani Kado ambapo timu hizo zilitoka sare kwa kufungana mabao 2-2.
Posted by MROKI On Tuesday, September 23, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo