Nafasi Ya Matangazo

September 21, 2014

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Mlandizi, Kibaha Vijijini, ambapo alisema kua CCM itaanza kuwafukuza viongozi wabovu na wala rushwa. Kinana yupo mkoani Pwani kuimarisha uhai wa chama, kuhimiza, na kusukuma utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia kaaikia wananchi kuhusu tika mkutano wa hadhara Mlandizi, Kibaha Vijijini, ambapo aliwananga wapinzania kwamba wanahangaika na maandamano wakati CCM wanawahangaikia mandeleo ya wananchi.
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Mwinshehe Mlao wakiondoka baada ya kufungua jengo la CCM Wilaya Kibaha Vijijini
 Kinana akisaidia kupaka rangi alipokagua jengo la Baraza la Ardhi la Kata ya Mlandizi iliyojengwa kwa msaada wa Diwani wa Kata hiyo, Euphresia Kadala (kushoto)
 Kinana akihutubia baada ya kufungua jengo la Baraza la Ardhi la Kata ya Mlandizi
 Kinana akipanda mti wa kumbukumbu alipotembelea Kituo cha Afya cha Mlandizi
 Kinana akizungumza baada ya kushiriki ujenzi wa jengo la kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya cha Mlandizi
 Kinana akipandisha bendera wakati wa uzinduzi wa shina la wakereketwa wa Kikundi cha Mshikamano Mlandizi Mjini
 Nape akimbusu mtoto Ashrafu Waziri wa mkazi wa Mlandizi wakati wa ziara kuimarisha uhai wa chama Kibaha Vijijini
 Wafuasi wa CCM, wakisikiliza kwa makini wakati Kinana akihutubia wakati wa uzinduzi wa shina la vijana la mshikamano Kibaha Vijijini. Kutoka kulia ni Flaviana Juma, Moureen Willfred na Fadhila Jumanne
 Kinana akikagua mradi wa maji katika Kijiji cha Bokomnemela Kibaha Vijijini
 Kinana akiagana na Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Dk. Hashim Mohamed baada ya kukagua mradi wa maji katika Kijiji cha Bokomnemela.
 Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani, Joyce Masunga akihutubia katika mkutano huo
 Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini, Hamoud Jumaa akielezea kuhusu miradi mbalimbali iliyotekelezwa katika jimbo hilo kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
 Mkazi wa Mlandizi akiuliza swali katika mahakama ya wazi ya Kinana katika kutano huo
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza akijibu swali la mwananchi aliyelalamikia kitendo cha waalimu kuwafukuza wanafunzi waliokosa kutoa michango shuleni ambapo Kinana alikemea vitendo hivyo.
 Baadhi ya wanachama wa Chadema wakionesha kadi baada ya kujiunga na CCM katika mizikutano uliofanyika Kibaha Mlandizi
Wanachama wapya wakila kiapo baada ya kukabidhiwa kadi za chama  hicho
Posted by MROKI On Sunday, September 21, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo