Nafasi Ya Matangazo

May 13, 2014

DSC_0051
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Zanzibar (Muungano na Utawala Bora), Mh. Mwinyi Haji Makame, akisaini kitabu cha maombolezo mara baada ya kuwasili kuhudhuria misa maalum ya kumwombea aliyekuwa Balozi wa Malawi nchini, Mh Flossie Gomile Chidyaonga kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).
DSC_0063
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Zanzibar (Muungano na Utawala Bora), Mh. Mwinyi Haji Makame akibadilishana mawazo na Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Dk Ishaya Samaila Majanbu (kushoto).
DSC_0099
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. John Haule na kulakiwa na Makamu Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mh. Chisiza.
DSC_0106
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akisubiri kwenda kutia saini kitabu cha maombolezo kabla ya kuanza kwa ibada maalum ukumbini hapo. Kushoto ni Makamu Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mh. Chisiza.
DSC_0110
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akisaini kwa huzuni Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini, Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga kilichotokea Hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salaam tarehe 09 mei 2014. Kulia ni Makamu Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mh. Chisiza.
DSC_0116 DSC_0123
Balozi wa Finland Tanzania, Sikka Antila wakilia kwa uchugu pamoja na Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Bi .Joyce Mends-Cole wakati wa misa maalum ya kumwombea aliyekuwa balozi wa Malawi nchini Tanzania Mh. Flossie Gomile Chidyaonga kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.
DSC_0124  DSC_0131
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akisalimiana na Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Bi .Joyce Mends-Cole. Katikati ni Balozi wa Finland Tanzania, Sikka Antila.
DSC_0138
Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Bi .Joyce Mends-Cole (mwenye mtandio mweupe) akibadilishana mawazo na baadhi ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania nje ya ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.
DSC_0146
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Balozi wa Malawi nchini Tanzania Flossie Gomile Chidyaonga ukiingizwa kwenye ukumbi tayari kuanza kwa ibada maalum na kutoa heshima za mwisho.
DSC_0167
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Balozi wa Malawi nchini Tanzania Flossie Gomile Chidyaonga.
DSC_0169
Mchungaji akiongoza ibada maalum ya kumwombea marehemu Flossie Gomile Chidyaonga.
DSC_0184
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Bi. Tonia Kandiero (kushoto) akiwa na baadhi ya mabalozi pamoja na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa Tanzania wakati wa ibada maalum ya kumwombea marehemu Flossi Chidyaonga iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.
DSC_0186
DSC_0189 DSC_0191
Nyuso za simanzi zikiwa zimetawala ukumbini hapo.
DSC_0192 DSC_0194 DSC_0197
Baadhi ya waombolezaji waliohudhuria ibada msiba wa Balozi Flossie Gomile Chidyaonga.
DSC_0198 DSC_0203
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard K. Membe (Mb) akiwa mwenye huzuni kubwa kwenye misa ya kumwombea marehemu Balozi Flossie Chidyaonga.
DSC_0206
Familia ya karibu ya marehemu ikiongozwa na Makamu Balozi wa Malawi nchini, Mh. Chisiza (kulia).
DSC_0219
Huzuni, simanzi na majonzi vilitawala ukumbini hapo.
DSC_0221
DSC_0222
DSC_0264
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akitoa mkono wa pole kwa ndugu wa karibu wa familia ya marehemu mara baada ya kutoa heshima za mwisho.
DSC_0277
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha-Rose Migiro akitoa mkono wa pole familia ya balozi Flossie Gomile Chidyaonga.
DSC_0284
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akitoa mkono wa pole kwa wafiwa.
DSC_0289
DSC_0299
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Bi. Tonia Kandiero, akitoa mkono wa pole kwa wafiwa.
DSC_0308
Balozi wa Zambia hapa nchini, Mhe. Judith Kangoma Kapijimpanga, akishindwa kujizuia wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga.
DSC_0318
Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Mh. Filiberto Sebregondi, akitoa heshima zake za mwisho.
DSC_0324
DSC_0327
DSC_0333
Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Bi .Joyce Mends-Cole, akitoa pole kwa wafiwa.
DSC_0382
DSC_0387
DSC_0394
DSC_0380
DSC_0410
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania , Mizinga Melu,(wa tatu kulia) , Balozi wa Zambia hapa nchini, Mhe. Judith Kangoma Kapijimpanga (wa pili kulia) wakati wa misa maalum ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga.
DSC_0407
Posted by MROKI On Tuesday, May 13, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo