Nafasi Ya Matangazo

May 24, 2013

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KIUONGO wa Yanga, Haruna Niyonzima leo ameongeza mkataba ndani ya klabu yake kwa kujifunga kwa miaka miwili zaidi na kuwafurahisha wapenzi na wanachama wa timu yake.
 
Haruna Niyonzima wa pili kutoka kushoto, wakati anatambulishwa na uongozi wa Yanga, baada ya kupigwa pini kwa miaka miwili zaidi.

Wakati Niyonzima anazungumza na wanahabari leo Makao Makuu ya Yanga, nje kulikuwa kumezunguukwa na mashabiki na wanachama wa Yanga waliokwenda kusikiliza kinachoendelea.

Niyonzima aliishukuru Yanga na kuahidi kufanya kazi ya maana zaidi katika kuhakikisha kuwa anaitumikia timu yake kwa mafanikio makubwa zaidi.

Mchezaji huyo alizua gumzo kwa siku kadhaa baada ya mkataba wake kumalizika, hivyo timu kadhaa ikiwamo Simba kuonyesha nia ya kutaka kumnyakua akipige kwenye klabu zao.
Posted by MROKI On Friday, May 24, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo