Nafasi Ya Matangazo

May 25, 2013

Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipata maelezo ya maandalizi ya sherehe hizo toka kwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Profesa Joram Biswaro mara baada ya kuwasili Addis Ababa.
*********
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ni miongomi mwa marais wa bara la Afrika watakaohudhuria Sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja  wa  nchi za Afrika (AU) zinazo fanyika rasmi leo Jumamosi Mei 25, 2013 katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia. 

 Shamrashamra zimetawala kila pembe ya jiji la Addis, wakati viongozi wa nchi za Afrika wakiwasili mmoja baada ya mwingine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bole. 

 Muungano wa Afrika wakati huo ukijulikana kama OAU, ulizaliwa Mnamo Mei 25, 1963 jijini Addis Ababa, ukianza na nchi za 32 na baadaye nchi 21 zikajiunga miaka ilivyozidi kwenda, huku Afrika ya kusini ikijiunga kuwa mwanachama wa 53 mwaka 1994. 

Mwaka 2001 OAU iligeuzwa kuwa AU katika mkutano uliofanyika Lusaka, Zambia. Jumamosi hii kutakuwa na sherehe za kilele kuadhimisha miaka hiyo 50 ya AU na kuhudhuriwa na marais karibia wote wa Afrika. 

 Kauli mbiu ya sherehe za hapo kesho ni mjadala mkuu kuhusu ushirikiano wa nchi za Afrika na kuimarishwa kwa muungano huo. Mwenyekiti wa tume ya muungano huo, Dr Nkosazana Dlamini Zuma, anaseme kuwa hii itakuwa fursa kwa AU kujadili kuhusu uwezo wa bara hili na ambacho kinaweza kufikiwa katika miaka 50 ijayo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa alipowasili Ijumaa usiku  tayari kujiunga na viongozi wenzie wa nchi za Afrika katika sherehe za miaka 50  tangu kuanzishwa kwa Umoja  wa  nchi za Afrika (AU) zinazofanyika leo katika makao makuu ya umoja huo
Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiwasili Addis Ababa.
Posted by MROKI On Saturday, May 25, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo