Nafasi Ya Matangazo

October 02, 2012

NI KATIKA KUHITIMISHA KILELE CHA MSIMU WA SERENGETI FIESTA 2012.

Lile tamasha kubwa kuliko yote hapa nchini, maarufu kama Serengeti Fiesta ambalo limekuwa likizunguka mikoa ya Tanzania bara na kufika takribani mikoa 11 sasa linaelekea katika kilele chake katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam siku ya jumamosi wiki hii ambapo msanii wa hiphop kutoka nchini Marekani Leonard Roberts maarufu kama Rick Ross atatumbuiza katika tamasha hilo.

Akizungumzia ujio wa msanii mkubwa kama huyo katika mahojiano maalum jijini Dar es Salaam leo, Meneja wa bia ya Serengeti bw. Allan Chonjo amesema tamasha la Serengeti Fiesta limekuwa likifanya vizuri sana katika mzunguko wake na kwamba watanzania wamekuwa wakifurahia uwepo wa tamasha hilo kutokana na mafanikio mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyapata kila ilipofika msimu  wa Serengeti Fiesta “mwaka huu tutakuwa na Rick Ross na kwamba watanzania waendelee kujenga imani na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia bia yake ya Serengeti Premium Lager, kwani kila kilele cha msimu wa tamasha hili ndio mwanzo wa maandalizi ya msimu unaofuata”.

Rick Ross ambaye ni mmoja kati ya wasanii wanaotamba sana katika miondoko ya kurap (hip hop) nchini marekani, atawasili hapa nchini siku ya alhamisi tayari kabisa kutumbuiza katika maadhimisho ya kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta siku ya jumamosi mwishoni mwa wiki hii.

Msimu wa Serengeti fiesta ulianzia katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Musoma, Shinyanga, Mwanza, Tabora, Singida, Dodoma, Morogoro, Mbeya na Iringa ambapo wakazi wake walipata burudani na ladha ileile ya bia ya Serengeti kabla ya kufikia mwisho  wa msimu wake wiki hii. Wasanii waliburudisha katika tamasha la Serengeti Fiesta nyanda za juu kusini ni pamoja na Inspector Haroun, Juma Nature, Roma Mkatoliki, Linah, Amini, Supa nyota Serengeti fiesta 2012 na wengine.

Maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na mikoa ya jirani wanatarijwa kumiminika katika viwanja vya Leaders Club kushuhudia burudani mbalimbali zitakazotolewa na wasanii wa hapa nchini, kabla ya kilele cha msimu wa ‘BHAAAS’ kumaliziwa na msanii Rick Ross na kundi lake kwa kiingilo cha shilingi 20,000/= za kitanzania kwa wale watakaonunua tiketi zao mapema na elfu 25,000/= kwa wale watakaonunu tiketi getini.

Katika tamasha la Serengeti Fiesta msimu wa uliopita uliokuwa ukijulikana kama ‘Haina Majotroo’ Kampuni ya bia ya Serengeti iliwaleta wasanii maarufu ambapo msanii wa muziki wa raga ‘Shaggy’ alitumbuiza katika uzinduzi wa msimu huo jijini Mwanza na msanii nyota kutoka nchini Marekani Ludacris alihitimisha msimu wa kwa kuwaburudisha wakazi wa jiji la Dar Es Salaam na majirani zake kama kawaida katika viwanja vya Leaders Club.

Umaarufu wa tamasha Serengeti Fiesta umekuwa ukitengeneza ajira mbalimbali za muda mfupi na kudumu, na pia nyingine zikianzishwa kupitia Serengeti Fiesta katika maeneo yote ambayo tamasha hilo lilipata kupita zikiwemo kuibuliwa kwa wasanii chipukizi na baadaye kujitegemea kimuziki, kujengeka kwa majina ya wasanii mbalimbali ambao hawakupata kufahamika zaidi kwa mashabiki wa muziki pamoja na kuibuka kwa wasanii wa filamu kupitia tamasha hili la Serengeti Fiesta,linalodhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti kupitia bia ya Serengeti Premium Lager.
Posted by MROKI On Tuesday, October 02, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo