Nafasi Ya Matangazo

May 09, 2012

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akipokewa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Tabora wakiongozwa na Mkuu wa mkoa huo Bi. Fatma Mwasa (aliyevaa kilemba)  na viongozi kutoka ofisi ya taifa ya Takwimu  mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa mkoa huo kwa ziara ya siku mbili ambapo pamoja na mambo mengine atafunga awamu ya kwanza ya kutenga maeneo ya  maandalizi ya Sensa ya watu na makazi  ya mwaka  2012 kitaifa katika viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora.
(Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.Tabora)
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akipata maelezo kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Tabora Bw. Mussa Chang’a (mwenye suti nyeupe) kuhusu  vikundi mbalimbali vya burudani vilivyokuwa vikitumbuiza wakati wa mapokezi yake mkoani Tabora.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwasa akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya mkoa wa Tabora kwa makamu wa rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Kulia ni waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal akizungumza na viongozi wa mkoa wa Tabora mara baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya mkoa huo ambapo ametoa wito kwa viongozi hao kufanya kazi kwa bidii na pia kuwahamasisha wananchi kushiriki katika sensa ya watu na makazi itakayofanyika nchi nzima kuanzia tarehe 26 mwezi Agosti.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (kushoto) akizungumza jambo na mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwasa(kulia) mjini Tabora.
 
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
 Tabora.
Makamu wa Rais  Dkt. Maohammed Gharib Bilal amewataka viongozi  kote nchini wawe mfano  wa kuigwa kwa kutoa ushirikiano na kukubali kuhesabiwa  wakati wa zoezi la sensa ya watu na makazi itakayofanyika  nchi nzima mwezi  Agosi  mwaka huu.
Akizungumza na viongozi wa mkoa wa Tabora leo mara baada ya kuwasili kwa ziara ya siku mbili Dkt. Bilal amesema  sensa ya watu na makazi ni muhimu kwa taifa  kwani itatoa mwelekeo wa nini cha kufanya kwa maendeleo ya taifa.
Amesema viongozi bila kujali nafasi walizonazo wanalojukumu kubwa la kuhahkikisha kuwa zoezi la sensa ya watu na makazi linafanyika kwa ufanisi mkubwa kutokana na mikakakati na maandalizi mazuri yaliyofanywa na ofisi ya taifa ya Takwimu.
Amefafanua kuwa  kila mtanzania ni mshiriki wa zoezi hilo huku akitoa wito kwa wananchi wote kujitokeza na kutoa ushirikiano siku ya sensa ili waweze kuhesabiwa katika maeneo yao.
“Sisi sote ni washiriki wa zoezi hili , sote lazima tukubali kuhesabiwa hivyo jukumu letu ni kuhamasishaba ili tuweze kuleta mabadiliko” amesema .
Ameongeza kuwa  upatikanaji wa takwimu   sahihi  za idadi ya watu na makazi pamoja na hali ya kiuchumi  utatoa dira ya upangaji wa mipango mizuri ya maendeleo ya taifa.
 Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwasa akitoa salaam za mkoa huo na taarifa ya utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo amesema  mkoa wake umepiga hatua kimaendeleo licha ya changamoto mbalimbali zilizopo.
Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na tatizo la ajira, bei za bidhaa kupanda mara kwa mara kutokana na ukosefu wa miundombinu inayoufungua mkoa huo na mikoa mingine pamoja na tatizo la upatikanaji wa maji ambalo ameiomba serikali kutekeleza mradi wa maji kutoka ziwa Victoria.
Aidha ameipongeza serikali kwa kuuchagua mkoa wa Tabora kuwa mwenyeji wa ufungaji wa awamu ya kwanza kitaifa ya kutenga maeneo ya maandalizi ya sensa ya watu na makazi itakayofanyika nchi nzima mwezi Agosti mwaka huu.
Ikumbukwe kuwa  zoezi lz sensa ya watu na makazi la mwaka huu litakalodumu kwa siku saba linafanyika ikiwa ni miaka 10 baada ya sensa  ya mwisho iliyofanyika mwaka 2002 wakati sensa nyingine zilifanyika nchini miaka ya 1967, 1978 na mwaka 1988.
Posted by MROKI On Wednesday, May 09, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo