Nafasi Ya Matangazo

August 02, 2010

Maonesho ya 88 mwaka 2010 yameanza kwa kishindo mjini Dodoma. Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko(WVBM) imejipanga kikamilifu kutoa huduma bora kwa muda wote wa maonesho. Tafadhali, usikubali kuhadithiwa, fika mwenyewe katika banda lao, ujionee.. Naibu Waziri wa Miundo mbinu Mh Hezekia Chibulunje na Mkuu wa Mkoa wa Singida Parseko Kone wakitembelea banda la WVBM.
Mgeni rasmi katika ufunguzi Mh Parseko Kone akipata maelezo kuhusu trekta jipya la kisasa lilitengenzwa na taasisi ya Camartec.
Mh Kone akitazama bidhaa zilizoletwa na taasisi mbali mbali katika maonesho hayo..
Mh Kone akipewa maelezo na mdau kutoka SIDO kuhusiana na bidhaa mbali mbali za taasisi hiyo.
Mwenyekiti wa TASO Dkt Engerbert Moyo (Kulia), akimuongoza Mh Kone kukagua banda la WVBM... Kati kati yao ni Mkurugenzi wa Sekta ya Viwanda Vidogo na vya kati katika WVBM Ndugu Desystant Massawe.
Picha kwa hisani ya Kitengo cha Habari na Mawasiliano, WVBM.

Posted by MROKI On Monday, August 02, 2010 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo