August 01, 2022

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA MEJA JENERALI SULEIMAN MZEE ATEULIWA MKUU WA MKOA WA MARA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara na kutengua uteuzi wa Dkt. Raphael Masunga Chegeni.

Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Suleiman Mzee alikuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP).

Uapisho utafanyika Ikulu Dar es Salaam, tarehe 1 Agosti, 2022.

No comments:

Post a Comment