September 14, 2016

KIWANDA CHA TANZANIA CHAONGOZA KWA UBORA BARANI AFRIKA



 Meneja wa kiwanda cha TBL Mbeya,Jemedari Waziri akiwakabidhi kombe la ushindi baadhi ya wafanyakazi waliofika uwanja wa ndege wa Songwe kumpokea akitokea nchini Afrika ya Kusini.
Mwonekano wa kombe la ushindi
 Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Mbeya wakiangalia kombe la ushindi
 Meneja Rasilimali watu wa kiwanda cha Bia cha TBL- Mbeya, Sarah Zayumba (aliyeshika kombe), akiwa ameshika kombe  hilo baada ya kuwasili katika kiwanda hicho.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha Bia cha TBL- Mbeya, wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa na kombe na cheti cha ushindi baada ya kiwanda hicho kutwaa tuzo ya kuwa kiwanda bora  na kushika nafasi ya kwanza Afrika kati ya viwanda 21 vya bia barani Afrika muda mfupi baada ya Meneja wa Kiwanda hicho, Jemedari Waziri kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe (SIA)-Mbeya akitokea Afrika ya Kusini. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

**************
WAKATI serikali ya awamu ya tano inajipanga kuifanya Tanzania nchi ya viwanda tayari dalili njema zimeishajitokeza kuwa watanzania tukiamua tunaweza kwa kuwa kiwanda kinachoshikilia rekodi ya ubora barani Afrika ni kiwanda cha kutengeneza Bia cha TBL kilichopo katika kitongoji cha Iyunga mkoani Mbeya.

Kwa mara nyingine tena baada ya kushindanishwa na  viwanda vikubwa vipatavyo 21 barani Afrika,mwishoni mwa wiki iliyopita TBL Mbeya imeibuka kinara na kutangazwa kuwa kiwanda bora barani Afrika kati ya viwanda vilivyopo chini ya kampuni kubwa yenye viwanda vya kutengeneza bia duniani ya SABMiller na kimelinda rekodi yake kilichokuwa kinaishikilia.

Rekodi hii inaenda sambamba na dhamira ya serikali ya kuifanya Tanzania nchi ya viwanda na inadhihirisha kuwa uwekezaji wa viwanda sio lazima ufanywe maeneo ya mijini kama ambavyo ilikuwa imezoeleka kwa muda mrefu.

Mhandisi Jemedari Waziri,Meneja wa kiwanda hiki akiongelea mafanikio haya alisema kuwa anajivunia ushindi huu kwa kuwa ni uthibitisho halisi kuwa watanzania tunaweza kufanya vizuri  na kuleta maendeleo kwa kasi tukiamua.

Tunaposema ubora wa kiwanda tunaamaanisha ubora wa bidhaa tunazozalisha,teknolojia tunazotumia,raslimali watu tuliyonayo,mchango wa kiwanda kwa serikali na jamii iliyotuzunguka bila kusahau utunzaji wa mazingira ambayo ni moja ya nguzo ya kampuni yetu”.Alisema.

Aliongeza kuwa ushindi huu ni kwa wana Mbeya wote na wana kanda ya Nyanda za Juu Kusini “Tunawashukuru wateja wetu wote kwa kutuunga mkono wakati wote na tutaendelea kuwaletea bidhaa bora kwenye soko na kubuni miradi mbalimbali ya kijamii itakayosaidia kuleta mabadiliko”.Alisema

Jemedari pia alisema ushindi huu unatokana na jitihada za pamoja kutoka kwa wafanyakazi wote wa kiwanda na TBL Group kwa jumla na anafurahi kuona kiwanda kinaendeshwa na watanzania asilimia kubwa ikiwa ni vijana wenye vipaji vya ajabu na waliobobea katika fani mbalimbali.

No comments:

Post a Comment