Nafasi Ya Matangazo

April 20, 2024

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza na Timu ya mpira wa miguu ya FGA ya mkoani Ruvuma.





Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ameitaka Timu ya mpira wa miguu ya FGA ya mkoani Ruvuma ambayo inashiriki Ligi Daraja la kwanza katika msimu huu wa mwaka 2023/24 iendelee kupambana na kufanya vizuri ili kucheza ligi hiyo msimu ujao.

Mhe.Ndumbaro ametoa kauli hiyo alipokutana na kuzungumza na timu hiyo Aprili 19, 2024 mjini Songea wakati timu hiyo ilipokua ikijiandaa kusafiri kwenda mkoani Mbeya kuikabili timu ya Mbeya City, Aprili 21, 2024.

Amewataka wachezaji wajiamini na kuonesha uwezo wao ili kuisaidia timu kusonga mbele pamoja na kuweka mazingira mazuri ya kujiuza katika soko la ndani na nje.

Aidha, Waziri Dkt. Ndumbaro amewasisitiza wachezaji hao wapambane ili  kupata alama sita muhimu kwenye michezo miwili iliyobaki ambapo mchezo wao wa mwisho utakuwa dhidi ya Ken Gold ya Jijini Mbeya ili wajihakikishie kubaki katika nafasi nzuri katika ligi hiyo.
Posted by MROKI On Saturday, April 20, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo