Nafasi Ya Matangazo

May 28, 2017

Na Woinde Shizza,Arusha
Kikosi cha Afc Arusha kimejinasibu kuwa kitawafunga mabigwa wa ligi kuu bara msimu uliomalizika  Timu ya  Yanga Afrika,katika mchezo wao wa kirafiki unaotajarajiwa kupichezwa Jumapili hii  May 28 katika kiwanja cha kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini hapa

Akiongea na gazeti hili kocha wa kikosi hichi kipya cha timu ya AFC Fikiri Elias  alisema kuwa vijana wake wapo tayari kuwapatia burudani wapenzi wa ke wa soka mkoani hapa huku akiwapa sifa viongozi wa serikali kwa kuwa begakwa bega katika kuhakikisha soka la mkoa wa Arusha linarudi katika ramani yake
Alisema kuwa japo hii ni mechi yao ya kirafiki baina yao na timu ya Yanga lakini watatumia mchezo huu pia kuangalia kikosi bora ambacho kitakaa kambini kwa ajili ya kuandaa timu ya kikosi kitakacho unda AFC mpya itayoshiriki ligi daraja la kwanza .

,, pamoja ya kuwa timu ya yanga inawachezaji wazoefu wengi na pia ndio wametoka tu kutwaa ubigwa mara ya tatu lakini napenda kusema hivi japo mechi hii ni ya kirafiki lakini nimeaada kikosi kizuri nanauhakika lazima tutaifunga timu hii ili tuweke historia japo ni mechi ya kirafiki ,,alisema Fikiri

Kwa upande wake kocha msaidizi  timu ya  Yanga ambao wameshikilia ubigwa  kwa mara ya tatu mfulukizo ligi kuu bara  Juma Mwambusi alisema kuwa mchezo huu ni muhimu  kwao kwani ni moja  ya program zao katika kujiandaa kuelekea katika michuzano inayowakabili  ikiwemo mashindano ya Sport Pesa

Kikosi hichi cha yanga kipo katika ziara ya kutembeza kombe lake kwa mashabiki wa mikoani ambapo mkoa wa Arusha umekuwa wa kwanza kuona kombe hilo na wakitoka mkoani hapa wanampango wa kulipeleka mkoani Dodoma ,ambapo pia wanajangwan hawa wamekuwa ni timu ya tatu kuoka ligi kuu bara msimu ulioisha kutoa katika aridhi ya jiji la Arusha iliyokuwa na ukame wa timu za ligi kuu mara baada ya timu za Ruvu shooting na Simba  zilizowaikutua hapa katika mtanange wake ulioisha

Akizungumzia mchezo huo wa kirafiki  mmoja wawaandaaji wa mechi hiyo ambayo katibu wa timu ya AFC  Charles Mwaimu alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika timu zote zipo tayari wanaisubiri tu siku ya mechi ifike.

Aliwasihi wananchi wa mkoa wa Arusha na pembezoni kujitokeza kwa wingi kuishabikia timuyao ya AFC ikiwa ni ujio mpya wa timu hii mara baada ya kupotea kwa muda ,na aliwasihi wananchi wa mkoa wa Arusha kujitokeza kuwapa morali wachezaji wao .

Aidha alisema kuwa pia mbali na mechi hii ya yanga kucheza na AFC pia wanampango wa timu hii kwenda mkoani manyara kucheza mechi baida yao na timui ya Merirani.
Posted by MROKI On Sunday, May 28, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo