Nafasi Ya Matangazo

July 05, 2016



 Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group wakionyesha medali zao muda mfupi baada ya kumalizika kwa matembezi




Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group na familia zao katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kumalizika kwa matembezi yaliyotayarishwa na taasisi ya Ocean Church.

WAFANYAKAZI wa kampuni ya TBL Group wamepongeza hatua ya kampuni kutekeleza mpango wa Afya kwanza ambao unawawezesha kujua hali ya afya zao wakiwa kazini,kujengewa mazingira ya kufanya mazoezi na familia zao na  kupatiwa ushauri wa jinsi gani ya kukabiliana na changamoto za magonjwa ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi nchini.

Wakiongea baada ya kumaliza kushiriki mbio za kilometa 5 zilizotayarishwa na taasisi ya Ocean  Church na kufanyika jijini Dar es Salaam  baadhi yao walisema kuwa utaratibu huu ni wa muhimu wa kuwawezesha kushiriki katika mazoezi kwa ajili ya kuweka afya zao na familia zao vizuri.

Akiongea kwa niaba ya  wafanyakazi wenzake baada ya kumalizika zoezi hilo la utekelezaji wa progamu ya Afya Kwanza Sam Mhagama kutoka TBL Ilala alisema kuwa mpango huu ni mzuri kwa kuwa unawawezesha wafanyakazi kujenga utamaduni wa kupima afya  zao mara kwa mara,kupata ushauri wa kitaalamu na kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao.
Kwa upande wake Seleman Mbena alisema kuwa utaratibu wa kusogeza huduma za afya sehemu za kazi  na kufanya mazoezi ni mzuri kwa kuwa unawawezesha wafanyakazi kupata elimu ya kujikinga na maradhi mbalimbali na wale wanaosumbuliwa na maradhi wanapata elimu ya jinsi ya kukabiliana nayo pia wanapata elimu ya lishe bora na jinsi ya kukabiliana na changamoto ya magonjwa hasa yanayosababishwa na maisha ya kisasa wanayoishi wafanyakazi wengi.

Mratibu wa Programu ya Afya Bora wa kampuni ya TBL Group,Julieth Mgani alisema Japo suala la afya limekuwa halipewi kipaumbele na waajiri wengi nchini lakini  ni suala muhimu la kuzingatiwa na waajiri wengi ili kuleta tija na ufanisi, kwa kuwa wafanyakazi wenye afya bora wanashiriki vizuri katika shughuli za uzalishaji

Alisema Afya Bora kwa wafanyakazi haina maana  wafanyakazi kulipiwa gharama za matibabu mahospitalini na waajiri wao bali  inahusisha mambo mengi kuhusiana na afya zao na afya za familia zao.

Mgani alisema Alisema katika sehemu  za kazi suala la Afya linapaswa kuzingatiwa wakati wote sio kulipa kipaumbele mara chache wakati wa kuadhimisha siku ya Afya au ya ugonjwa fulani kama ambavyo imekuwa mazoea kufanyika na siku hiyo ikipita hakuna kinachoendelea.
Posted by MROKI On Tuesday, July 05, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo