Nafasi Ya Matangazo

March 23, 2016

Mwenyeki wa kamati John Nayopa akimkabidhi Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo,Taarifa ya kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa Nyamongo na Kampuni ya mgodi wa dhahabu ya Acacia North Mara, 
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo,akionesha taarifa aliyokabidhiwa na Kamati hiyo ambapo ameahidi kuisoma na kuitolea majibu yanayostahili ndani ya kipindi cha wiki tatu tangu Machi 23,2016 alipokabidhiwa taarifa hiyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Nyamongo na Kampuni ya mgodi wa dhahabu ya Acacia North Mara, John Nayopa, akisoma taarifa ya utekelezaji wa kamati hiyo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini( hayupo pichani)
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, akizungumza jambo mara baada ya kupokea Taarifa ya utekelezaji kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara  na Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara.
Meza kuu ikimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati( hayupo) akitoa taarifa ya utekelezaji ya Kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara  na Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara, kutoka kushoto waziri wa nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga, Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche.
Sehemu ya wajumbe kutoka Serikali za vijiji wakisikiliza taarifa ya  kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara  na Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara, kutoka Serikali ya kijiji. 
Sehemu ya wajumbe kutoka Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara, wakisikiliza taarifa ya Kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara  na Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara. KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Sehemu ya ya wanakamati wakisikiliza taarifa ya utekelezaji kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya kushughulikia mgogoro kati ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara  na Mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia wa North Mara.
******************
Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo amepokea ripoti maalumu ya kumaliza mgogoro wa wananchi wa Nyamongo na mgodi wa wa dhahabu wa Kampuni ya Acacia North Mara uliodumu kwa miaka 6 sasa. Anaandika Zuwena Msuya-Wizara ya Nishati na Madini.

Akizungumza mjini Tarime Mkoani Mara baada ya kupokea ripoti hiyo Prof. Muhongo ameshauri wananchi wa Tarime kuwa watulivu wakati akiendelea kuisoma ripoti hiyo na kutolea majibu mambo yalioyo andikwa katika riporti hiyo.

Profesa Muhongo alisema anaimani mambo yote yalioandikwa katika ripoti hiyo ni mawazo ya wananchi waliohojiwa na  atashangaa endapo kuna mtu atajitokeza  kuikataa.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya Tarime,Glorious Luoga alisema ripoti hiyo itatoa majibu stahiki kwa wanaohitaji kulipwa na hata wasiostahili hivyo wananchi wakae tayari kupokea utekelezaji wa ripoti baada ya kusoma na kupitishwa na Waziri.

 Naye Mbunge wa Tarime vijijini John Heche alisema kuwa anaimani na ripoti hiyo kuwa itatenda haki kwa wananchi wake wa Nyamongo ili kutimiza  ahadi ya Rais aliyoitoa wakati akiomba kura kuwa hatamaliza kabisa tatizo la Nyamongo lililodumu kwa muda mrefu.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhandisi John Nayopa alisema kamati hiyo imepokea malalamiko zaidi ya 4400 ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi,malalamiko ambayo yalilenga masuala ya fidia ya ardhi,athari za shughuli za mgodi hasa upande wa mazingira,uvamizi wa mgodi,sakata la tegesha na Askari kutuhumiwa na kunyanyasa na kutesa wananchi.

Kamati hiyo iliundwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo mwezi mmoja uliopita ina wajumbe 27,19 wataaalamu wa Serikali, na Wenyeviti wa vitongoji 80.
Posted by MROKI On Wednesday, March 23, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo