Nafasi Ya Matangazo

March 23, 2016

Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari mda mfupi uliopita katika ukumbi wa mikutano wa wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwezi Machi mwaka huu, ambapo Mapato ya Kodi (TRA) shilingi 1,283,274,000,000. Mapato yasiyo ya kodi ni shilingi 77,504,000,000. Mapato yatokanayo na vyanzo vya halmashauri ni shilingi 43,490,000,000 Jumla ikiwa ni 1,404,268,000,000. Pia amesema kuwa Serikali inatarajia kupata mikopo na misaada ya mifuko ya Basket na Miradi ya maendeleo kutoka kwa washirika wa maendeleo shilingi 71,200,000,000.
 Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari mda mfupi uliopita jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Ashantu Kijaji akiwa katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo.

Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

UFAFANUZI WA
MAPATO NA MATUMIZI YA SERIKALI KWA MWEZI MACHI, 2016
A:  MAPATO 
(i)Mapato ya kodi (TRA) shilingi 1,283,274,000,000
(ii)Mapato yasiyo ya kodi shilingi 77,504,000,000
(iii)Mapato yatokanayo na vyanzo vya Halmashauri shilingi 43,490,000,000 
Jumla shilingi 1,404,268,000,000
(iv)Tunatarajia pia kupata mikopo na misaada ya mifuko ya Basket na miradi ya maendeleo kutoka kwa washirika wa maendeleo shilingi 71,200,000,000
B: MATUMIZI
1.  Mishahara
(a)Watumishi wa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa shilingi 484,057,177,680 ikijumuisha malimbikizo ya shilingi 9,479,389,384 na hasa kwa walimu katika Halmashauri 154
(b)Watumishi wa Taasisi na Wakala za Serikali shilingi 97,985,822,320 ikijumuisha malimbikizo ya shilingi 518,822,320 kwa Taasisi na Wakala 24 na hasa sehemu kubwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jumla ya mishahara ni shilingi 582,043,000,000
  
2.           Posho ya chakula kwa ajili ya vyombo vya ulinzi na usalama shilingi 43,556,500,000.
3.         Ruzuku ya Vyama vya Siasa shilingi 1,433,583,000
4.         Posho ya Madaktari wanafunzi 1608 shilingi 1,721,000,000.
5.         Wizara ya Afya Ununuzi wa madawa na vifaa tiba shilingi 2,597,961,000
6.         Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa semista ya tatu shilingi 57,040,000,000
7.         Kutekeleza mpango wa Elimu bure shilingi 18,777,000,000
8.         Mapato ya ndani kwa Halmashauri kwa ajili ya miradi na uendeshaji wa ofisi shilingi 43,490,000,000
9.         Madeni ya watumishi wasio walimu katika Halmashauri  shilingi 3,618,900,612
10.      Miradi ya umeme shilingi 73,252,000,000
-            Wakala wa Umeme Vijijini shilingi 24,020,000,000
-            Mradi wa Umeme Kinyerezi I shilingi 43,800,000,000
-            Mradi wa kufua umeme makambako – Songea shilingi 5,482,000,000
11.      Malimbikizo ya madeni ya Makandarasi wa barabara shilingi 166,905,919,730
12.      Miradi ya Maji shilingi 10,951,000,000
13.      Mfuko wa Reli shilingi 2,651,000,000
14.      Fidia kwa wananchi kupisha mradi wa Kurasini Trade and Logistic Hub shilingi 3,048,904,930
15.      Mradi wa Ununuzi wa dawa na vifaa Tiba (ORIO) shilingi 2,106,657,644

16.      Mfuko wa kuchochea maendeleo ya jimbo shilingi 5,124,997,500
Posted by MROKI On Wednesday, March 23, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo