Nafasi Ya Matangazo

June 25, 2015

Mratibu wa Kipindi cha Diaspora,Maggid Mjengwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya kipindi cha Diaspora kitachoanza kuruka katika kituo cha TBC hivi karibuni katika ukumbi wa idara ya Habari Maelezo,Kushoto ni Mkurugenzi wa Diaspora Intiative,Emmanuel Mwachullah,Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Rosemary Jairo.
 ****************
ATANZANIA walioko Ughaibuni wanatakiwa kuelezwa vitu ambavyo vitawafanya watanzania nchini kutambua umuhimu wa watu katika masuala mbalimbali ikiwemo uchumi.
 
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya habari  Maelezo  jijini ,Dar es Salaam,Mratibu wa Watu Waishio Ughaibuni (Diaspora),Majjid Mjengwa amesema kutokana na kutambua uwepo watu milioni mbili wako  nje nchi ambao wanatakiwa kushirikishwa katika masuala mbalilmbali yanayoendelea nchini.
 
Mjengwa amesema kutokana na kuona hilo amebuni kipindi cha Diaspora katika kituo cha TBC kwa ajili ya kuelimisha watanzania juu watu wanaoishi  nje  ya nchi  juu ya faida kwa watu hao.
 
Amesema katika kipindi hicho kitatoa mwanga kwa watu wa ughaibuni na watanzania nchini juu kushirikiana katika masuala mbalimbali.
 
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nchi na Ushirikiano wa Kimataifa,Rosemary Jairo amesema kuwa ubunifu wa mjengwa wa kipindi cha Diaspora kitasaidia kuelimisha watanzania juu maana wakishajua itakuwa ni rahisi kupata uraia pacha.
 
Amesema watanzania wengi hawajui faida ya kuwa na watu nje ya nchi katika masuala ya uchumi wanawezaje kuchangia kuleta maendeleo.
Jairo amesema kuna watanzania  wanafanya kazi ughaibuni wanafanya vizuri hali ambayo wanaweza kufanya katika nchi yao.
Posted by MROKI On Thursday, June 25, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo