Nafasi Ya Matangazo

May 06, 2015

 Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi akionyesha sehemu ya vitabu kabla ya kukabidhi msaada wa vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya milioni 4/-, kupitia Mradi wa ‘Airtel Shule Yetu’ kwa Shule ya Sekondari ya King’ongo iliyopo Kimara katika Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam jana. Waliokaa (kutoka kushoto) ni Meneja wa Airtel Tawi la Kinondoni, Fadhili Mwasyeba, Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Godfrey Mheluka na Mkuu wa Shule hiyo, Nyaibuli Bhoke.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari ya King’ongo, Godfrey Mheluka (kulia), akikabidhi msaada wa vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya milioni 4/-, kwa Mkuu wa Shule hiyo, Nyaibuli Bhoke baada ya kukabidhiwa na Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto), kupitia Mradi wa ‘Airtel Shule Yetu’ katika hafla iliyofanyika shuleni hapo Kimara jijini Dar es Salaam jana.
 Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (wa pili kushoto), akikabidhi vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya milioni 4/-, kupitia Mradi wa ‘Airtel Shule Yetu’ kwa baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya King’ongo, katika hafla iliyofanyika shuleni hapo Kimara jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia (kutoka wa pili kushoto)ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo, Godfrey Mheluka, Afisa Elimu na Takwimu wa Manispaa ya Kinondoni, Omary Ahmed na Mkuu wa Shule hiyo, Nyaibuli Bhoke .
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya King’ongo wakifurahia vitabu vya masomo ya sayansi, baada ya Kampuni ya Airtel kupitia Mradi wake wa  ‘Airtel Shule Yetu’ kukabidhi vitabu vyenye thamani ya milioni 4/- kwa shule hiyo katika hafla iliyofanyika shuleni hapo Kimara jijini Dar es Salaam jana.
Posted by MROKI On Wednesday, May 06, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo