Nafasi Ya Matangazo

June 28, 2012

"There is no more lovely, friendly and charming relationship, communion or company than a good marriage".

KUMI NA TANO SI HABA (PONGEZI)
Pongezi nina zituma, kwako Tedi nawe Nesto
Mu imara kama chuma, kwa upendo wake Kristo
Mungu awape uzima, mkalea na watoto,
Kumi na tano si haba, Mroki nawapongeza.

Mroki nawapongeza, kumi na tano si haba,
Nesto leo umeweza, nyumbani waitwa baba,
Tedi  ye hakuteleza, tuli yeye hakuyumba,
Kumi na tano si haba, Kidevu nawapongeza.

Mungu kawabariki, wana weri kawapa,
Japo home hamshikiki, ulizi wana huwapa,
Ibada mnashiriki, pongezi mi ninawapa,
Kumi na tano si haba, Kidevu nawapongeza.

Kubwa shukrani kwa mola, mja wetu wa karima,
Alo ziepusha hila, kwetu sisi maamuma,
Tedi waivaa shela, hakupenda dada wema,
Kumi na tano si haba, Kidevu nawapongeza.

Jala wetu wa Jalalu, wape zaidi hekima,
Mmoja asiwe lulu, mwingini akawa Kima,
Hapo hawatafaulu, kuheshimiana daima,
Kumi na tano si haba, Kidevu nawapongeza.

Wote mkajidhatiti, kwenye wenu upendo,
Mkipiga Serengeti, msipigane mabindo,
Kuweni watu wa geti, upole uwe mtindo,
Kumi na tano si haba, Kidevu nawapongeza.

Hizi saba zinatosha, kiu kimenikamata,
Sio vyema kuwachosha, maneno mmeyapata,
Nami nitajibidisha, yenu siri kuipata,
Kumi na tano si haba, Kidevu nawapongeza.

Mroki Mroki “Father Kidevu
+255 717 002303

"Marriage: a book of which the first chapter is written in poetry and the remaining chapters written in prose
Posted by MROKI On Thursday, June 28, 2012 1 comment

1 comment:

  1. AnonymousJune 28, 2012

    Hongera dada ni makubwa sana Mungu akubariki sana

    ReplyDelete

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo