Nafasi Ya Matangazo

March 25, 2012

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Injinia Stella Manyanya akipanda kwenye ndege inayomilikiwa na Kampuni ya Auric Air Services Ltd leo katika uwanja wa ndege wa Mwl. J.K. Nyerere Dar es Salaam kama ishara ya kuzindua rasmi huduma ya safari za anga kutoka Dar es Salaam kwenda Sumbawanga Mkoani Rukwa itakayoendeshwa na Kampuni hiyo, huduma hiyo haikuwepo hapo kabla. Kampuni hiyo itakuwa inaendesha safari zake siku ya Jumatano na Jumapili ambapo gharama za safari hiyo kwenda na kurudi itakuwa Dola za Kimarekani 370$ sawa na takriban Tshs 598,000/= kwenda na kurudi. Wanaoshuhudia ni Katibu Mkuu Utumishi GeorgeYambesi, Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hillal, Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa kampuni ya Huduma za Ndege ya Auric Air Services Ltd Deepesh Gupta na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Salum Mohammed Chima.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya akimkabidhi Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa kampuni ya Huduma za Ndege ya Auric Air Services Ltd Deepesh Gupta zawadi ya Ua na Kadi kama pongezi na shukrani kwa kampuni hiyo kwa kuanzisha huduma ya safari za ndege za abiria kutoka Dar es Salaam-Sumbawanga Mkoani Rukwa kupitia Mbeya leo katika uwanja wa ndege wa Mwl. J.K. Nyerere Dar es Salaam. Kampuni hiyo itakuwa inaendesha safari zake siku ya Jumatano na Jumapili ambapo gharama za safari hiyo kwenda na kurudi itakuwa Dola za Kimarekani 370$ sawa na takriban Tshs 598,000/= kwenda na kurudi. Wanaoshuhudia ni Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Salum Mohammed Chima, Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hillal na Katibu Mkuu Utumishi George Yambesi.


Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akipanda ndege ya Kampuni ya Auric Air ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa huduma hiyo kwa safari ya kuelekea Sumbawanga Mkoani Rukwa leo.

Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini (CCM) Aeshi Hillal alikuwa sehemu ya abiria 13 waliopanda ndege hiyo leo Jijini Dar es Salaam kuelekea Sumbawanga Mkoani Rukwa katika uzinduzi wa huduma hiyo. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa kwa ushirikiano na Mbunge huyo pamoja na wadau wengine ndiyo matunda ya muwekezaji huyo Mkoani Rukwa.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi George Yambesi ambaye pia ni Mwanarukwa akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari na kuelezea furaha yake kwa kuanzishwa safari hizo.
Picha ya pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyanya akiwa na Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa kampuni ya Huduma za Ndege ya Auric Air Services Ltd Deepesh Gupta (kushoto kwake), Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Salum Mohammed Chima (kushoto), Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hillal (kulia) na Katibu Mkuu Utumishi George Yambesi muda mfupi kabla ya kuondoka katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam leo kuelekea Sumbawanga Mkoani Rukwa katika sherehe za uzinduzi wa huduma hiyo.
Ndege ya Auric Air itakayoendesha huduma za anga za kampuni hiyo ikiwa katika maandalizi ya safari ya leo kutoka Dar es Salaam kwenda Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Source: http://rukwareview.blogspot.com
Posted by MROKI On Sunday, March 25, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo