August 07, 2026

DKT. JAKAYA KIKWETE AVUTIWA NA UBUNIFU WA KILIMO MSETO NA UFUGAJI WA KISASA KATIKA BANDA LA KIBAHA DC NANE NANE 2026

 

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,  Agosti 7, 2026, ametembelea Banda la Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha katika Maonesho ya Wakulima Nanenane Kanda ya Mashariki 2026 yanayoendelea mkoani Morogoro na kuvutiwa na ubunifu mbalimbali unaooneshwa katika banda hilo.

Akiwa katika ziara hiyo, Dkt. Kikwete alipata fursa ya kujionea teknolojia ya kilimo mseto (Integrated Farming) inayolenga kuongeza tija kwa wakulima wenye maeneo madogo kwa kuunganisha shughuli za kilimo, ufugaji na matumizi bora ya rasilimali zilizopo.

Pia alivutiwa na ufugaji wa ng’ombe aina ya Sahiwal, ambao ni ng’ombe wenye uwezo mkubwa wa uzalishaji wa maziwa na wanaofaa kwa mazingira ya Tanzania. Katika maelezo yaliyotolewa na wataalamu wa banda hilo, Dkt. Kikwete alifurahishwa zaidi na simulizi ya kijana anayejishughulisha na ufugaji huo wa kisasa.

Halmashauri inaendelea kuwakaribisha wananchi, wadau, wawekezaji na wananchi wote kutembelea banda lake ili kujionea fursa, ubunifu wa kilimo na ufugaji, vivutio vya kipekee pamoja na huduma mbalimbali zinazotolewa.


No comments:

Post a Comment