May 04, 2026

ZIARA YA KIKAZI YA RAIS WA JAMHURI YA KENYA, MHESHIMIWA WILLIAM SAMOEI RUTO, NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa William Samoei Ruto, anatarajiwa kuwasili nchini leo, tarehe 04 Mei, 2026, kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili. 

Akiwa nchini, Rais Ruto atafanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kabla ya viongozi hao kuongoza mazungumzo rasmi ya pamoja kati ya ujumbe wa Tanzania na Kenya, na kuzungumza na waandishi wa habari.

 Mazungumzo hayo yataangazia jitihada za kuimarisha ushirikiano wa kindugu na kimkakati kati ya Tanzania na Kenya katika biashara, uwekezaji, miundombinu, usafirishaji na maeneo mengine ya maslahi ya pamoja. 

Viongozi hao pia wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa Hati za Makubaliano na Mikataba ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya, pamoja na kushiriki Jukwaa la Biashara litakalowakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchi zote mbili. 

Aidha, siku ya Jumanne, tarehe 05 Mei, 2026, Rais Ruto anatarajiwa kuhutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mkoani Dodoma, ikiwa ni sehemu ya ziara yake. Siku hiyohiyo baadaye, atarejea nchini Kenya baada ya kuhitimisha ziara yake nchini.

No comments:

Post a Comment