Mameneja wa mikoa na vituo wa Wakala wa
Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kubadilisha mitazamo ya
watumishi na wanaopewa huduma na Wakala ili kuufanya kuwa mfano wa kuigwa na
Taasisi zingine za Umma.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) Moses R. Mabamba alipokuwa akizungumza na mameneja wa Mikoa na vituo katika kikao kilichofanyika Makao Makuu ya Wakala mjini Dodoma ambapo
amewaagiza mameneja hao kufanya kazi kwa bidii ili kutoa huduma bora kwa
Serikali na jamii kwa ujumla ambazo zitaifanya TEMESA iweze kuwa na uwezo wa
kutekeleza majukumu yake mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa maslahi bora ya
watumishi.
KATIKA GAZETI TANDO HILI UTAWEZA KUJIPATIA HABARI MOTO MOTO KATIKA PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI KUTOKA NDANI NA NJE YA TANZANIA HASA YALE YANAYOGUSA MAISHA YA KILA SIKU YA MTANZANIA.LUGHA KUU INAYOTUMIKA HUMU NI KISWAHILI.

No comments:
Post a Comment