June 27, 2024

KATIBU MKUU WIZARA YA NISHATI AKUTANA NA UJUMBE WA UMOJA WA ULAYA (EU)










Dar es salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi  Mramba leo 26 Juni, 2024,  amekutana na kufanya mazungumzo na  Ujumbe kutoka  Umoja wa Ulaya (EU) wakiongozwa na  Cedric Merel, Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Ulaya ambapo mazungumzo yao yalijikita katika kujadili utekelezaji wa Programu ya Maboresho ya Sekta ya Nishati _(Energy Sector Reform Programme)_ inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya. 

katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Viongozi na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati, Wizara ya Fedha, EWURA, TANESCO,  NBS na REA. Ambapo EU   waliwasilisha vigezo vilvyokubaliwa katika kukidhi masharti ya kupatiwa fedha za utekelezaji wa kazi zilizopangwa. 

EU imeeleza kuwa vigezo hivyo vinahusisha kufanyiika kwa mijadala inayohusu sekta ya nishati, kuundwa kwa timu ya Wizara ya ufuatliaji wa miradi na kufanya tathmini, kupunguza upotevu wa umeme na kuendelea kuunganisha wateja wa umeme. 

Serikali kwa upande wake imewasilisha hatua zilizofikiwa katika kutimiza masharti hayo kwa mwaka wa Fedha 2023/24 ambapo EU watayapitia na kuyajadili ambapo  inategemewa kuwa fedha hizo zitapatikana mwisho wa mwaka wa fedha 2023/24.

No comments:

Post a Comment