October 04, 2023

ONESHO LA KIMATAIFA LA SITE 2023, KUPAMBWA NA WANYAMA HAI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Onesho la Kimataifa la Swahili International Tourism Expo (S!TE) katika ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Thereza Mugobi.Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Onesho la Kimataifa la Swahili International Tourism Expo (S!TE) katika ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb)(hayupo pichani) katika  kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam leo.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika picha ya pamoja na  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dunstan Kitandula (Mb)(wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Damas Mfugale (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Thereza Mugobi mara baada ya kikao na  waandishi wa habari kuhusu Onesho la Kimataifa la Swahili International Tourism Expo (S!TE) katika ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam leo.
***********

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki amesema kuwa maandalizi ya Onesho la saba la Utalii la Kimataifa la Swahili International Tourism Expo – S!TE 2023 yamekamilika ambapo  kwa mara ya kwanza kutakuwa na bustani ya wanyama hai
 
Akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari leo Oktoba 3, 2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam amesema onesho hilo litafanyika kuanzia Oktoba 6 - 8 mwaka huu ambapo wageni na wadau muhimu wa sekta kutoka maeneo mbalimbali duniani watahudhuria.
 
“Katika kipindi chote onesho hili limekuwa jukwaa muhimu na lenye ushawishi kwa wadau mbalimbali ndani na nje ya nchi walio katika mnyororo wa huduma za utalii.” Amefafanua Mhe. Kairuki
 
Waziri Kairuki amewataja baadhi ya wadau watakaoshiriki kwenye maonesho ya mwaka huu kuwa ni pamoja na Mabalozi wa nchi mbalimbali, Bodi za Utalii kutoka nchi za Afrika zikiwemo Uganda na Malawi, Waoneshaji (Exhibitors) zaidi ya 100 kutoka ndani na nje ya nchi. Wanunuzi wa biashara za utalii (Buyers) zaidi ya 70 kutoka katika masoko yetu ya Kimkakati ya kimataifa hususan, Ulaya, Amerika na Asia.
 
Aidha, amesema onesho la mwaka huu litapambwa na Bustani ya Wanyamapori hai ili kuwavutia watembeleaji (visitors) na kuhamasisha Utalii wa ndani, pamoja na Jukwaa la Uwekezaji la Utalii (Tanzania Tourism Investment Forum-TTIF) na ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kuja kutembelea na kuona hazina na urithi wa utalii wa Tanzania pia
 
“Natoa rai kwa watanzania, wawekezaji, na wadau wengine wa utalii kushiriki kikamilifu onesho la SITE 2023, ambalo ni fursa ya muhimu kukutana na wadau wenzenu waliopo katika mnyororo wa thamani wa Sekta ya Utalii, ili kwa pamoja tuhakikishe sekta hii inapiga hatua tukitambua melengo makubwa tuliyonayo ya kufikia watalii milioni 5 na mapato ya Dola za Marekani Bilioni 6 ifikapo mwaka 2025. Halikadhalika kuendelea kuitangaza nchi yetu kimataifa kupitia utambulisho wetu wa Tanzania, Unforgettable na Programu ya Tanzania – The Royal Tour.” Amesisitiza Mhe. Kairuki.
 
Waziri Kairuki ametoa wito  kwa  wadau mbalimbali  kutembelea  mtandao wa site.tanzaniatourism.go.tz ili kuona  mambo  muhimu yanayohusu  onesho hili ikiwa ni pamoja na  semina mbalimbali, midahalo inayoangazia mada za utalii na fursa za uwekezaji ambapo amesema Kauli mbiu ya Onesho la S!TE 2023 ni: Utalii Unaowajibika kwa Maendeleo Jumuishi.

“Natoa rai kwa watanzania, wawekezaji, na wadau wengine wa utalii kushiriki kikamilifu onesho la SITE 2023, ambalo ni fursa ya muhimu kukutana na wadau wenzenu waliopo katika mnyororo wa thamani wa Sekta ya Utalii, ili kwa pamoja tuhakikishe sekta hii inapiga hatua tukitambua melengo makubwa tuliyonayo ya kufikia watalii milioni 5 na mapato ya Dola za Marekani Bilioni 6 ifikapo mwaka 2025. Halikadhalika kuendelea kuitangaza nchi yetu kimataifa kupitia utambulisho wetu wa Tanzania, Unforgettable na Programu ya Tanzania – The Royal Tour.” Amesisitiza Mhe. Kairuki.
 
Waziri Kairuki ametoa wito  kwa  wadau mbalimbali  kutembelea  mtandao wa site.tanzaniatourism.go.tz ili kuona  mambo  muhimu yanayohusu  onesho hili ikiwa ni pamoja na  semina mbalimbali, midahalo inayoangazia mada za utalii na fursa za uwekezaji ambapo amesema Kauli mbiu ya Onesho la S!TE 2023 ni: Utalii Unaowajibika kwa Maendeleo Jumuishi.

No comments:

Post a Comment