July 15, 2015

MAKADA WA CCM PIJEI NA WAKILI NAWERA WACHUKUA FOMU KUWANIA JIMBO LA KAWE

Wakili Elias Nawera akionyesha alama ya dole baada ya kukabidhiwa fomu hizo. Kulia ni mgombea ubunge mkoa wa Dar es Salaam kupitia Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Lilian Mkosani.
 Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe (kushoto), akimkabidhi fomu ya kugombea ubunge jimbo la Kawe, kada wa chama hicho, Wakili Elias Nawera (katikati), Dar es Salaam leo mchana. Kulia ni mgombea ubunge mkoa wa Dar es Salaam kupitia Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Lilian Mkosani
 Wakili Nawera (kulia), akiandika jambo kabla ya kulipa sh. 100,000  ya kuchukulia fomu.
 Kada wa CCM Jumaa Mhina 'Pijei' (katikati), akipokea fomu ya kuwania ubunge Jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam, kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe leo mchana. Anaye shuhudia kulia ni Kada wa chama hicho anayewania ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia CCM, Ramadhan Ndanga 'Potipoti'.
 Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Sheshe (kushoto), akimpa maelezo ya kufuata baada ya kukabidhiwa fomu hizo.

No comments:

Post a Comment