Nafasi Ya Matangazo

May 06, 2024

Fedha za Mfuko wa Jimbo zimeendelea kuleta tija na matokeo chanya katika kuimarisha na kukuza uchumi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla na hivyo kuleta manufaa kwa wananchi wa pande zote mbili za Muungano.
 
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Wingwi Mhe. Omar Issa Kombo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingir) Mhe. Dkt. Selemani Jafo leo tarehe 06 Mei, 2024 bungeni.
 
Katika swali lake Mhe. Kombo alitaka kujua lini Serikali itafanyia kazi changamoto ya Kodi na Tozo kwenye Fedha za Mfuko wa Jimbo kwa upande wa Zanzibar, Naibu Waziri Katambi amesema kuwa kodi na tozo hutozwa kwa mujibu wa Sheria pindi bidhaa au huduma zinapotolewa au kununuliwa.
 
Aidha, amebainisha kuwa bidhaa na huduma zinazotolewa hukatwa kodi ya zuio la kodi (With Holding Tax) kwa kuzingatia Sheria ya Kodi ya Mapato, Sura ya 332 chini ya kifungu cha 83 (1) (c) kwa malipo ya ada ya kwa huduma kwa ajili ya utoaji wa huduma ya kitaalamu na kifungu (83 A) malipo kwa bidhaa zinazotolewa na mkazi wa uendeshaji biashara.
 
Naibu Waziri Katambi amesema kuwa kodi hutozwa kwa kuzingatia Sheria ya Manunuzi inayotumika Zanzibar inayojulikana kama sheria zinazotolewa na mkazi wakati wa undeleshaji biashara.
Posted by MROKI On Monday, May 06, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo