Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 27 Agosti, 2021 amepokea Hati za Utambulisho wa Mabalozi wawili walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini.
Mabalozi
waliowasilisha Hati za Utambulisho ni Mhe. Zahra Ali Hassan Balozi wa Somali na Mhe. Nabil Hajlaoui Balozi wa
Ufaransa wote wakiwa na makazi yao hapa nchini.
Akizungumza
mara baada ya kupokea hati hizo, Mhe. Rais Samia amewapongeza Mabalozi hao na
kuwaomba kufikisha salamu zake kwa viongozi wakuu wa nchi zao na kusisitiza
kuwa Tanzania itaendeleza uhusiano na ushirikiano kwa manufaa ya pande zote.
Kwa
upande wao Mabalozi hao wamempongeza Mhe. Rais Samia kwa utendaji mzuri na
kumuahidi ushirikiano.
Mabalozi
hao wameeleza kuwa mataifa yao yana dhamira ya dhati ya kuimarisha uhusiano
katika sekta mbalimbali hususan biashara na uwekezaji.
Wakati huohuo, Mhe. Rais Samia
amemuapisha Mhe. Balozi Togolani Edriss Mavura kuwa Balozi wa Tanzania nchini
Korea Kusini.
Pia,
Mhe. Rais Samia amemuapisha Bw. Mathew Modest Kilama kuwa Katibu wa Tume ya
Utumishi wa Umma.
Hafla
hiyo ya uapisho ilioyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma imehudhuriwa na
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa,
Mawaziri, Makatibu Wakuu, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka pamoja na
viongozi mbalimbali wa Serikali.
0 comments:
Post a Comment