Nafasi Ya Matangazo

September 02, 2019

 Mbunge wa jimbo la Same Magharibi, Dk. Mathayo David Mathayo akikabidhi Mabati 200 kwa uongozi wa kata ya Vudee kama alivyoahidi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na zahanati ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi yam waka 2015-2020 mbele ya wananchi wa kata hiyo
Mbunge wa jimbo la Same Magharibi  Dk.Mathayo David Mathayo akimkabidhi diwani wa kata ya Bangalala, George  Mshana mipira kwa ajili ya ligi itakayoshindanisha vijiji vyote ambapo mshindi kwa upande wa wanawake atapatiwa shilingi milioni mbili na wanaume timu mshindi atapatiwa shilingi milioni mbili wakati wa mkuatano wa hadhara ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya utekelezaji wailani ya uchguzi ya CCM mwaka 2015-2020 kama alivyoahidi kwa jailia ya kata hiyo. 
 Mbunge wa jimbo la Same Magharibi Dk.Mathayo David Mathayo akimkabidhi fedha taslim diwani wa kata ya Bangalala George  Mshana mbele ya wananchi wa kata hiyo wakati wa mkuatano wa hadhara ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya utekelezaji wailani ya uchguzi ya CCM mwaka 2015-2020 kama alivyoahidi kwa jailia ya kata hiyo. 
 Mbunge wa jimbo la Same Magharibi, Dk Mathayo David Mathayo akikabidhi mifuko ya saruji kwa uongozi wa kata ya Vudee kama alivyoahidi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na zahanati ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020 mbele ya wananchi wa kata hiyo
 Mbunge wa jimbo la Same Magharibi Dk. Mathayo David Mathayo akiwakabidhi fedha za ujenzi wa madarasa,ununuzi wa viti na mahitaji mengine walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari wa kata ya vudee Bukuri Masago na diwani wa kata hiyo Vudee Ngomoi Ntarishwa ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020 kama alivyoahidi kwa jaili ya kusaidia maendeleo ya elimu katika kata hiyo. 
Mbunge wa jimbo la Same Magharibi Mathayo David Akihutubia wananchi wa kata ya Vudee katika jimbo la Same Magharibi wakati wa ziara yake katika kata hiyo ikiwa ni mfululizo wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi alizoahidi.
***************
MBUNGE wa jimbo la Same Magharibi Dk.Mathayo David Mathayo ameendelea na ziara yake ya kutekeleza ilani ya uchaguzi katika jimbo lake huku akija na staili mpya ya kutatua kero za wananchi kwa mtindo wa papo kwa papo.

Licha ya kutekeleza ahadi alizoahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwaongoza wananchi wa Same Magharibi mbunge huyo amekuwa akitekeleza wakati mwingine kutoa fedha taslim  pale anapoombwa na wananchi wa kata husika nje ya ahadi anazotekeleza katika kila kata.

Akizungumza na wananchi wa kata ya Vudee na Bangalala mbele ya mbunge huyo diwani wa Kata hiyo Ngomoi Ntarishwa pamoja na kumshukuru mbunge huyo kwa utekelezaji wa ahadi zote alizoahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwaongoza wanachi hao.

“mhe mbunge wananchi wa Vudee wanakushukuru sana kwa utekelezaji wa ahadi uliahidi na umetekeleza,sisi wanannchi wa Vudee tuna Imani kubwa na wewe hivyo pamoja na kuwa umetelekeza bado tuna changamoto kadhaa ambazo tunaomba pia utusaidie”alisema Ntarishwa
Mbunge huyo ambae licha ya kutekeleza ahadi za mabilioni amekuwa akipandwa na mzuka pale wananchi wake wanapomlilia shida na kuhakikisha hawaachi hivyo hivyo wala kuahidi bali amekuwa akizitatua papo kwa papo.

“Ndugu zangu leo nimekuja kutekeleza ahadi zote nilizoahidi wakati nilipokuja kuwashukuru kwa ushindi wa kishindo ambao mlinichagua,lakini nasikia kuna watu wanapitapita wakisema kuwa Mathayo hajarudi,hivi niwaulize swali ilani inatekelezwa ndani ya kipindi gani,si ni kwa miaka mitano?hivi mtoto akiaanza shule akafika kidato cha pili utasema basi kabla hajafika kidato cha nne?,” alizungumza kwa kuhoji Mathayo.

Mathayo amewataka wananchi hao  kutokubali kurubuniwa na kuendelea kuwa na Imani na chama cha mapinduzi ambacho kupitia Rais John Magufuli kimeleta maendeleo makubwa kwa wananchi wake tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani.

Akiwa katika kata ya Vudee na Bangalala mbunge huyo ametekeleza ahadi zake kwa kutoa mifuko ya fedha taslimu saruji  350 kwa ajili ya ujenzi wa shule,zahanati,vyoo vya wanafunzi,,mabomba ya maji,mabati 200,matanki ya maji,comyuta,mashine za photokopi,mipira ya kuchezea,key bord,nondo,meza na viti,huku akiahidi kuleta katapila kwa ajili ya ujenzi wa barabara korofi ya Kisesa,vyote kwa ajili ya kata ya Vudee.

Baadhi ya ahadi mpya alizozitoa na kuzitatua papo kwa papo katika kata ya Vudee ni kompyuta,mashine ya photokopi,jiko la shule ya sekondari masheka,mabati 30,na upande wa zahanati ya kiji cha kisesa bati 100.

Ombi jingine alilolitekeleza papo kwa papo katika kata ya Bangalala ni kukubali kutoa gari la kubebea wagonjwa kwa ajili ya kata hiyo, kuleta katapila kwa ajili ya kutengeneza barabara za kata hiyo,tenki la kuhifadhia maji,ambapo pia ametoa fedha taslimkwa ajili ya kunua mipira ya maji 20 na nyinginezo.
Posted by MROKI On Monday, September 02, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo