Nafasi Ya Matangazo

March 21, 2019

Mkurugenzi Mtendaji wa Arusha United Sports Club Otte Beda Ndaweka
TIMU ya Arusha United Sports Club, inayoshiriki ligi daraja la kwanza imetangaza kujitoa rasmi katika ligi hiyo kwa madai  ya kuchoshwa na vitendo ambavyo si vya kimichezo huku TFF kupitia bodi ya ligi ikishindwa kuchukua hatua stahiki.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mkurugenzi Mtendaji wa timu hiyo Otte Beda Ndaweka amesema kuwa licha ya timu hiyo kuwa katika nafasi nzuri katika kundi B imeona si buasara kuendelea na ligi hiyo kufuatia matukio mbalimbali ikiwemo kufanyiwa vurugu wakati ikicheza na timu kadhaa tangu timu hiyo ianze kushiriki ligi hiyo msimu wa mwaka 2018-2019.
Aidha Ndaweka amesema licha ya timu hiyo kuwa na vibali vya kurekodi michezo yake yote ya ligi kuanzia mchezo wake dhidi ya Dodoma Fc uliofanyika mjini Dodoma bodi hiyo pia imeshindwa kuhakikisha maelekezo,miongozo au vibali vyake vinaheshimiwa na au kuchukua hatua pale ambapo haviheshimiwi.
Timu ya Arusha United ni moja ya timu zinazoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara kwa kundi B,kwa sasa ikiwa imekwisha cheza michezo 17 kukusanya jumla ya point 28 huku ikishika nafasi ya tano ambapo timu ya Geita gold FC ikiongoza ligi hiyo ikiwa na point 33.
Posted by MROKI On Thursday, March 21, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo