Nafasi Ya Matangazo

February 14, 2019

Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bi. Neema Mwanga (kulia) kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, akitoa maelezo kuhusu uzingatiaji wa Sheria, taratibu na Kanuni katika utekelezaji wa kazi za Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakati wa kikao cha wadau wa mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Mkoa wa Kilimajaro, Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi Aisha S. Amour, akifuatiwa na Katibu Tawala Msaidizi– Mipango Bi. Lydia Liwa (kushoto). 
Baadhi ya wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia kwa makini mada iliyotolewa na Msajili wa NGOs nchini kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Bi. Neema Mwanga (hayupo pichani) kuhusu uzingatiaji wa Sheria, taratibu na Kanuni katika utekelezaji wa kazi za Mashirika yasiyo ya Kiserikali mkoani humo. 
Mkurugenzi Msaidizi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bi. Tausi Mwilima (kulia) kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto- Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, akielezea faida za NGOs kusajili ndani ya Sheria ya NGO Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005 wakati wa kikao cha wadau wa Mashirika hayo kilichofanyika Mkoani Kilimajaro, wengine ni Msajili wa NGOs Bi. Neema Mwanga (wa tatu kushoto), akifuatiwa na Katibu Tawala Msaidizi– Mipango Bi. Lydia Liwa (wa pili kushoto) na  (Kushoto) ni Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Kilimanjaro B. Hilda Lauwo .
Msajili wa Mashirika Yasiyo Ya kiserikali Bi. Neema Mwanga (wa pili kulia) kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akihakiki cheti  cha usajili cha moja ya Mashirika aliyoyatembelea wakati wa ziara ya kufuatilia uratibu wa NGOs katika mkoa wa Kilimanjaro.
**************
Na Mwandishi wetu Kilimanjaro
Vyanzo vya mapato ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali sio siri kwa kuwa fedha hizo zitafutwa kwa kutumia majina na taarifa za wanajamii hao hivyo fedha za mradi zinapoatikana isiwe siri katika utumikaji wake.

Hayo yamesemwa na Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kutoka Wizara ya Afya- Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto B. Neema Mwanga alipofanya kikao na wadau wa Mashirika ya NGOs wanaofanya kazi zao katika wilaya zote za Mkoa wa Kilimanjaro.
Bi Mwanga amewaagiza wamiliki wa Mashirika hayo kote nchini kuhakikisha kuwa taarifa za vyanzo vya fedha vinakuwa wazi ili wanajamii waweze kuzifahamu na kutumika kwa mujibu wa andiko la maombi ya rasilimali hizo. 
“Vyanzo vya mapato ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali sio jambo la siri, tunapoandaa maandiko ya miradi yetu tunatumia taarifa za majina ya wananchi walioathirika katika maeneo husika hivyo Mashirika hayo kuficha taarifa za fedha hii sio haki”. Alisema.
Msajili ameongeza kuwa kila Shirika Lisilo la Kiserikali sharti liwe na Sera ya uendeshaji wa Shirika husika na Kanuni za maadili pamoja na Sera ya kuzuia kushwa mahala pa ili kuhakikisha kuwa Shirika linalinda maslahi ya taifa na kukuza haki  na utu wa wanajamii wanaonufaika na miradi inayotekelezwa.
Msajili huyo ameelekeza uongozi wa Mashirika hayo kuhakikisha yanafanya tafiti ili kujua na tathmini ya matatizo ya kijamii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Serikali kabla ya kuomba fedha kutoka kwa wahisani kwa lengo la kutekeleza miradi inayozingatia vipaumbele vya kitaifa na mahitaji ya makundi mbalimbali katika jamii zetu.    
Ameongeza  kuwa Mashirika hayo yanaowajibu wa  kuwa na daftari la mali za shirika ambazo zimenunuliwa na kulitunza ipasavyo na daftari hilo litaboreshwa kila mara ili kuhakikisha kuwa  mali zote za Shirika  zinahuishwa ili kukuza udhibiti wa mali hizo.
Aidha, Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ametoa agizo kwa wadau wa NGOs kuhakikisha wanawasilisha taarifa za mwaka na kulipa ada kwa wakati. 
Aidha ameongeza kuwa taarifa za fedha zitakazowasilishwa ziwe zimekaguliwa ili kutoa taswira ya halisi ya mapato ya Shirika kulingana na miradi iliyopokea fedha. 
Posted by MROKI On Thursday, February 14, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo