Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt aliyemtembelea akiwa ameongozana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke, na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuonesha albamu ya picha Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt inayoonesha Shule ya Sekondari ya Ihungo iliyobomolewa kabisa na tetemeko la ardhi Setemba 10, 2018 ambayo imejengwa upya na serikali ya Uingereza kupitia mpango wake wa maendelo ya elimu kupitia UKAid/DFID. Picha hizo zinaonesha shule hiyo baada ya tetemeko, wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi siku ya mwaka mpya wa 2017 na inavyoonekana sasa baada ya kujengwa upya. Mhe. Mordaunt, ambaye yuko nchini kwa ziara ya kikazi, alimtembelea Rais Dkt. Magufuli akiwa ameongozana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke, na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018
Uingereza
imetoa msaada wa shilingi Bilioni 307.5 kwa Tanzania kwa ajili ya kuunga mkono
juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
katika elimu, mapambano dhidi ya rushwa na uboreshaji huduma za afya.
Waziri
wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza Mhe. Penny Mordaunt ametangaza msaada
huo leo tarehe 10 Agosti, 2018 alipokutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Rais
Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mhe.
Penny Mordaunt amesema fedha hizo zinatolewa kwa ajili ya kuunga mkono
vipaumbele vya Mhe. Rais Magufuli ambapo kati yake shilingi Bilioni 124.5
zitaelekezwa katika kuinua ubora wa elimu hususani kutoa fursa ya elimu kwa
watoto wa kike na wenye ulemavu, shilingi Bilioni 23.5 zitaelekezwa katika
kuunga mkono juhudi za kupambana na rushwa, na shilingi Bilioni 160
zitaelekezwa katika kuboresha huduma za afya.
“Tunafanya
hivi ili kudhihirisha dhamira yetu ya kuimarisha na kukuza zaidi uhusiano na
ushirikiano wetu, tunataka kujielekeza katika kuhakikisha Mhe. Rais Magufuli
anafanikisha ahadi zake kwa Watanzania na tunafurahi kuwa wadau muhimu wa hilo”
amesema Mhe. Penny Mordaunt.
Ameongeza
kuwa pamoja na kuwa wachangiaji wakubwa katika bajeti ya Serikali, Uingereza ni
nchi inayoongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania na kwamba wanafurahishwa na wito
wa Mhe. Rais Magufuli kuwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara zaidi kutoka
Uingereza watakaowekeza kwa manufaa ya pande zote (win-win).
Mhe.
Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Penny Mordaunt kwa msaada huo na amemuomba
kufikisha shukrani zake kwa Waziri Mkuu wa Uingereza Mhe. Theresa May kwa
mchango mkubwa ambao Uingereza hutoa kuchangia bajeti ya Serikali na kufadhili
miradi mbalimbali ya maendeleo.
“Namshukuru
sana Waziri Penny Mordaunt kwa kutambua juhudi zetu za kuinua elimu, kupambana
na rushwa na ufisadi pamoja na kuboresha huduma za afya, msaada huu utatusaidia
kuongeza nguvu kwa sababu watoto wakipata elimu bora, tukikomesha rushwa na
watu wetu wakiwa na afya njema tutaweza kujenga viwanda na kukuza uchumi wetu
kwa kasi zaidi” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe.
Rais Magufuli amemuahidi Mhe. Penny Mordaunt kuwa fedha zilizotolewa kiasi cha
shilingi Bilioni 307.5 zitatumika vizuri na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano
itahakikisha uhusiano wa Tanzania na Uingereza unazidi kuimarishwa kwa kuwa
inatambua kuwa Uingereza ndio mwekezaji mkubwa hapa nchini na imekuwa ikitoa
misaada mikubwa ya fedha za walipa kodi wa Uingereza kwa ajili ya maendeleo ya
Tanzania.
Pia,
Mhe. Rais Magufuli amemkabidhi Mhe. Penny Mordaunt albamu ya picha za shule ya
sekondari Ihungo mkoani Kagera iliyojengwa upya baada ya kuharibika vibaya
kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 2016, na ameishukuru Uingereza
kwa msaada wa shilingi Bilioni 6zilizotumika kujenga majengo hayo kupitia
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).
Mazungumzo
hayo yamehudhuriwa na Balozi wa Uingereza hapa nchini
Mhe. Sarah Cooke na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.
Dkt. Augustine Mahiga ambaye amesema ziara ya Waziri Penny Mordaunt imezidi
kukuza uhusiano wa Tanzania na Uingereza.
0 comments:
Post a Comment