Nafasi Ya Matangazo

May 14, 2018

Shirika la Ndege linaloongoza Tanzania, Precision Air, leo hii limeshiriki katika jitihada za kuhifadhi mazingira katika maeneo ya hifadhi ya Mlima Kilimanjaro.


Katika kutimiza zoezi hilo, wafanyakazi wa shirikika hilo wakishirikiana na wanakijiji wa kijiji cha Ngarony pamoja na wafanyakazi wa wilaya ya siha wakiongozwa na Mkurugenzi mtendaji wa Wilaya ya Siha,Onesmo Buswelu wamefanikishaa upandwaji wa miti 1000 (elfu moja) katika eneo linalotenganisha kijiji cha Ngarony na hifadhi ya mlima Kilimanjaro.

 Akizungumzia tukio hilo Meneja Masoko na Mawasiliano wa Precision AirHillary Mremi amesema, Precision Air inatambua inawajibu wa kuutnza mlima Kilimanjaro kwani mlima huo una mchango wa moja kwa moja katika shughulli za shirika hilo.
 “Mlima Kilimanjaro unatutunza vyema sisi kama shirika na kama taifa kupitia utalii, hivyo sote tunawajibu wa kuutunza mlima huu na mazingira kwa ujumla wake.” Mremi aliongeza. 


Precision Air imekua ikifanya safari zake ndani ya mkoa wa  Kilimanjaro kwa zaidi ya miaka ishirini na nne (24) na kama mdau mmojawapo wa utalii, limefanya zoezi la upandaji wa miti ikiwa ni moja ya jitihada zake za kuhakikisha jamii inayo uzunguka mlima inaendelea kufaidika na uwepo wa mlima, amboa ni moja ya kivutio muhimu cha utalii nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Siha, Siha Valerian, amesema kuwa Shirika la Ndege  la Precision Air limeonyesha mfano wa kuigwa na wadau wengine wa mazingira na utalii. 
 
Valerian Ameongeza kuwa ni wakati sasa wa kuchukua hatua madhubuti kulinda mazingira yetu ili vizazi vijavyo viweze kufaidika na uzuri wa nchi yetu wa vivutio kama mlima Kilimanjaro na vingine.


Mlima Kilimanjaro  ndio mlima mrefu zaidi barani Afrika, ukiwa na urefu wa takribani mita 5,895 kutoka katika usawa wa bahari, pia ndio mlima mrefu zaidi duniani uliosimama wenyewe (Bila kutegemea kanda za milima).  

Shirika la Ndege la Precision Air lilianzishwa mwaka 1993 kama shirika binafsi la ndege za kukodi, likifanya safari zake kusafirisha watalii katika vivutio vya utalii kama Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Bonde la Ngorongoro pamoja na Visiwa vya Zanzibar.
Sasa Shirika hilo lenye makoa yake makuu katika Jiji la Dar es Salaam limeendelea kukua na kuwa moja ya mashirika yanayo heshimika katika ukanda wa Africa Mashariki na Africa kwa ujumla.


Ikifanya safari zake kutokea Dar es Salaam, Precision Air inasafiri kuelekea Arusha, Bukoba, Kilimanjaro, Mtwara, Mwanza, Tabora, Kahama, Zanzibar,Nairobi na Entebbe.
Posted by MROKI On Monday, May 14, 2018 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo