Nafasi Ya Matangazo

January 19, 2018

Mwandishi Wetu, TJNCDF
Shirikisho la Vyama vya Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza Tanzania (TANCDA) linaeleza kuwa karibu kila mtu anakabiliwa na tatizo la msongo wa mawazo.

Kinachosababisha hali hiyo, TANCDA inaeleza kuwa ni hali ya jumla ya maisha. Mazingira na mifumo ya maisha ambayo jamii inaishi yanachagiza binadamu kujikuta anapata msongo wa mawazo.

Kuna mambo mengi yanayoweza kumsababishia mtu kuwa na msongo, na hapa TANCDA inayaelezea kwa mfumo wa maswali.

Katika maswali hayo ukiona miongoni yanakuhusu, unapaswa kuchukua tahadhari ili tatizo la msongo wa mawazo lisikusababishie madhara.

Siyo rahisi mtu kujua madhara anayopata kama yanatokana na msongo wa mawazo yanayomkabili kwa sababu hiyo TANCDA inashauri jamii kuchukua tahadhari.
Miongoni mwa maswali mtu anayoweza kujiuliza ni: Je, hatuwi na wasiwasi kuwa watu wanachunguza ngua tunazovaa?

Je, hatushikwi na hofu pale tunapovuka barabara kuwa tunaweza kugongwa na magari? Je, hatuwi na wasiwasi pale tunaposhindwa kumaliza kazi zetu kwa wakati? BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI MAKALA HAYA.


Hayo ni baadhi tu ya maswali ambayo mtu anaweza kujiuliza. Jambo ambalo mtu anapaswa kulizingatia ni kuwa jambo lolote linalomsababisha mtu kuwa na hofu, woga, taharuki, kukosa raha au kushindwa kutekeleza majukumu mengine ni sehemu ya mambo yanayomsababishia msongo wa mawazo.

Je, tunapojikuta katika hali hii tufanye nini? TANCDA inashauri njia rahisi za kukabiliana na msongo wa mawazo ni kufanya mazoezi mara kwa mara na kuwa makini na jambo moja kwa wakati mmoja.

Njia nyingine, TANCDA inaeleza ni kumueleza mtu wako wa karibu na unayemuamini kuhusu tatizo lako ili akusaidie kwa ushauri.

Hali nyingine ya kukabiliana na msongo wa mawazo ni kucheka na kushiriki kwenye michezo, sherehe na burudani kama vile harusi, ubatizo na mikusanyiko ya dini.

Mtu anapaswa kujifunza kukubali kuwa hawezi kushindwa kila kitu na kutojitwika mambo mengi kuliko anavyoweza kufanya kwa wakati.

Kuwa na muda wa utulivu kwa dakika kadhaa na TANCDA inakushauri ni vyema ukachukua muda dakika chache kila siku kwa kuzima simu hasa pale inapokufanya uwe na majukumu mengi.


Makala haya yameandaliwa na Chama cha Waandishi Wanaopambana na Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza (TJNCDF). Maoni, ushauri au maswali tuma tjncdf@gmail.com au S.L.P 13695, Dar es Salaam.
Posted by MROKI On Friday, January 19, 2018 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo