Nafasi Ya Matangazo

January 29, 2018

Busi la kampuni Ya Tahmeed lenye namba za usajili T483 BFL limeungua moto katika Kijiji cha Kabuku wilayani Handeni mkoani Tanga. 

Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, SACP Edward Bukombe alisema basi hilo ambalo lilikuwa na abiria 9 tu kutoka Dar es salam liliungua moto kutokana na hitilafu za umeme. 

Alisema Dereva wa bus hilo Bakari Said (34) alihisi halipo vizuri katika mfumo wa engine akasimamisha gari kisha kuwaomba abiria washuke.

Hata hivyo hakukuwa na mtu aliyejeruhiwa kutokana na ajali hiyo. Hii ni mara ya pili kwa basi la kampuni hiyo kupata hitilafu Kwenye mfumo wa injini na kuungua moto.
Posted by MROKI On Monday, January 29, 2018 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo