Nafasi Ya Matangazo

November 20, 2017

1
Mgeni Rasmi Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Deus Sokoni akifungua mjadala katika Siku ya Kukumbuka waathirika wa Ajali Duniani (The World Day Of Remembrance For Road Traffic Victims 19 November 2017) iliyoandaliwa na kufanyika kwenye ofisi za Chama Cha Mbio za Magari Tanzania AAT Upanga jijini Dar es salaam ikishirikisha wadau kutoka taasisi mbalimbali nchini Tanzania
Wadau mbalimbali wamekutana na kujadiliana namna ya kupunguza ajali hasa katika kuzipitia sheria za usalama barabarani na kuzifanyia marekebisho pamoja na kuwakumbusha watumiaji wa Barabara kuzingatia sheria za usalama barabarani, Taasisi zilizoshiriki katika mjadala huo ni WHO, KIkosi Cha Usalama Barabarani, SUMATRA, Chama Cha Mbizo za Magari Tanzania AAT, Chama cha Kutetea Abiria Tanzania CHAKUA, TIRA na wawakilishi Idara ya Habari Maelezo.
2
Mratibu wa Semina hiyo Bw. Alferio Nchimbi akizungumza katika semina hiyo na kukaribisha wadau mbalimbai ili kuchangia michango yao katika mada mbalimbali zilizowasilishwa.
3
Mgeni Rasmi Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Deus Sokoni akisisitiza jambo wakati akijibu maswali katika semina hiyo kulia ni Mratibu wa Semina hiyo Bw. Alferio Nchimbi.
4
Bw. Monday Likwepa Katibu Mkuu wa Chama cha Kutetea Abiria akichangia mada katika semina hiyo.
5
Bi Mary Kessi Mratibu Programu ya Usalama Barabarani WHO akitoa mada katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ofisi za Chama cha Mbio za Magari Tanzania (AAT) Upanga jijini Dar es salaam.
6
Afisa Leseni Mwandamizi kutoka SUMATRA Bw. Gabriel Anthony akitoa mada katika semina hiyo.
7
Daktari Bingwa wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharura na Ajali Muhimbili Dk Juma Mfinanga akitoa ufafanuzi kwa upande wa hospitali ya Muhimbili wakati wa semina hiyo.
8
Baadhi ya washiriki wakiwa katika semiha hiyo
9 10
Posted by MROKI On Monday, November 20, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo